Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zaidi ya shilingi bilioni 127.7 Zatumika Kufikisha Nishati Vijijini Mwanza
Iddy Mwema 54

Zaidi ya shilingi bilioni 127.7 Zatumika Kufikisha Nishati Vijijini Mwanza

Zaidi ya shilingi bilioni 127.7 zimetumika kupeleka huduma ya nishati safi Vijijini Mkoa wa Mwanza hali iliyochochea ukuaji wa uchumi na kuboreka kwa huduma za kijamii vijijini.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG) ambapo Wakala huo uliwasilisha mpango kazi pamoja na bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027.

 

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Mwanza pekee imetoa jumla ya shilingi Bilioni 127.7 ili kutekeleza miradi ya kupeleka umeme hadi vitongojini. Mafanikio haya makubwa yamechangiwa pia na wabia wa maendeleo, tunawapongeza na kuwashukuru sana.

 

Niendelee kuwataka wananchi waendelee kulinda miundombinu ya umeme kwa kuwa serikali na wabia hawa wa maendeleo wanaweka fedha nyingi sana. Lakini pia niendelee kuwahimiza wabia wa maendeleo pamoja na REA kuendelea kuwekeza zaidi katika nishati safi ya kupikia,” amesema Mhe. Mtanda.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema kuwa wabia hao wa maendeleo wamekuwa na imani kubwa na fedha wanazotoa katika utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini na ndio maana wanaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia REA katika utekelezaji wa miradi hiyo huku akiahidi kuwa Bodi yake itaendelea kuhakikisha kunakuwa na thamani ya fedha katika miradi inayotekelezwa na REA.

 

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amesema kuwa Wakala umewasilisha mipango na vipaumbele vyake kwa mwaka ujao wa fedha ili wabia hao waweze kuona maeneo wanayoweza kuendelea kushirikiana na Serikali kupitia REA katika kuendelea kuboresha maisha ya Wananchi.

 

“Pamoja na kazi kubwa inayofanyika katika kujenga miundombinu ya umeme, lakini lengo la msingi ni mwananchi wa kawaida aweze kuunganishiwa umeme na aweze kupata manufaa ya upatikanaji wa umeme.

 

Tumewasilisha mipango pamoja na vipaumbele katika bajeti yetu ijayo ambapo ni kuharakisha upatikanaji wa umeme kwenye vitongoji. Tumewapitisha pia wenzetu katika mpango wetu maalum wa kuwezesha na kuharakisha uunganishaji umeme majumbani,” amebainisha Mhandisi Saidy.

 

Mhandisi Saidy pia ameongeza baadhi ya mipango mingine iliyopangwa kutekelezwa na Wakala kwa mwaka ujao wa fedha ni pamoja na kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia vijijini, kuwezesha miradi ya nishati jadidifu na kuongeza ufanisi katika matumizi ya umeme na utumiaji wa umeme katika shughuli za maendeleo.

 

Mwenyekiti wa Wabia wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati (EDPG), Robert Hovde ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa kufikisha umeme vijijini.

 

“Katika kipindi cha miongo kadhaa nyuma, Tanzania imekuwa na maendeleo makubwa katika kufikisha umeme vijijini yaliyotekelezwa na REA. Miundombinu ya umeme inaonekana hali inayotia matumaini kufikiwa kwa mpango wa kuunganisha umeme wananchi wote. Tunawatakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Hovde.

 

 

 

Share

Print
«June 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
12
Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.

Read more
34567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top