Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza
Mohamed Saif 132

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Mhe. Mtanda mesema hayo Aprili 16, 2026 Ofisini kwake alipokutana na Bodi, Menejimenti ya REA pamoja na Wabia wa Maendeleo, wanaoshirikiana na Wakala huo kwenye utekelezaji wa miradi yao Nchini.

“Nishati ya Umeme ni Nishati Muhimu, uwekezaji kwenye Kilimo na Mifugo hauwezi kufanyika kama hakuna Umeme. Ninao Wanawake wawili ambao wana miradi wa kufuga kuku zaidi ya 30,000 kila mmoja. Bila ya Nishati ya Umeme mradi wao hauwezi kuwa bora na endelevu.

Uwepo wa umeme vijijini umechochea miradi mbalimbali kuibuliwa na kutekelezwa maeneo ya vijijini hali inayochochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa pamoja na mtu mmoja mmoja,” amesema Mhe. Mtanda.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA Mhandisi Jones Olotu, amesema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuwapa fursa Wabia hao wa Maendeleo kutembelea na kujionea miradi inayotekelezwa na Wakala.

“Wabia hawa tumekuwa tukishirikiana nao kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali na hivyo leo wameweza kuja kujionea utekelezwaji wa miradi ya nishati vijijini,” amesema Mhandisi Olotu.

Faraja Nyoni ambaye ni Msimamizi wa shamba la Mwasonge, ambao pamoja na shughuli zingine, wanafuga kuku zaidi ya 30,000, amesema kuwa uwepo wa umeme umeweza kuwasaidia kutekeleza mradi huo kisasa na kupunguza gharama za uendeshaji.

Amesema awali walikuwa wakitumia zaidi ya shilingi milioni nne kwa ajili ya kuweka mafuta ya jenereta kuendeshea shughuli zao katika mradi huo lakini kwa sasa wanatumia shilingi milioni moja tuu.

Naye Mhandisi Wiston Nnko ambaye ni mhandisi wa mradi wa kukausha dagaa kwa kutumia umeme jua kutoka kampuni ya Millenium Engineers ameshukuru na kuipongeza REA kwa kuweza kuwawezesha wawekezaji mbalimbali wakiwamo wao hali iliyowawezesha kuongeza thamani ya soko la dagaa.

 

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top