Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza
Mohamed Saif 210

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Mhe. Mtanda mesema hayo Aprili 16, 2026 Ofisini kwake alipokutana na Bodi, Menejimenti ya REA pamoja na Wabia wa Maendeleo, wanaoshirikiana na Wakala huo kwenye utekelezaji wa miradi yao Nchini.

“Nishati ya Umeme ni Nishati Muhimu, uwekezaji kwenye Kilimo na Mifugo hauwezi kufanyika kama hakuna Umeme. Ninao Wanawake wawili ambao wana miradi wa kufuga kuku zaidi ya 30,000 kila mmoja. Bila ya Nishati ya Umeme mradi wao hauwezi kuwa bora na endelevu.

Uwepo wa umeme vijijini umechochea miradi mbalimbali kuibuliwa na kutekelezwa maeneo ya vijijini hali inayochochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa pamoja na mtu mmoja mmoja,” amesema Mhe. Mtanda.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA Mhandisi Jones Olotu, amesema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuwapa fursa Wabia hao wa Maendeleo kutembelea na kujionea miradi inayotekelezwa na Wakala.

“Wabia hawa tumekuwa tukishirikiana nao kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali na hivyo leo wameweza kuja kujionea utekelezwaji wa miradi ya nishati vijijini,” amesema Mhandisi Olotu.

Faraja Nyoni ambaye ni Msimamizi wa shamba la Mwasonge, ambao pamoja na shughuli zingine, wanafuga kuku zaidi ya 30,000, amesema kuwa uwepo wa umeme umeweza kuwasaidia kutekeleza mradi huo kisasa na kupunguza gharama za uendeshaji.

Amesema awali walikuwa wakitumia zaidi ya shilingi milioni nne kwa ajili ya kuweka mafuta ya jenereta kuendeshea shughuli zao katika mradi huo lakini kwa sasa wanatumia shilingi milioni moja tuu.

Naye Mhandisi Wiston Nnko ambaye ni mhandisi wa mradi wa kukausha dagaa kwa kutumia umeme jua kutoka kampuni ya Millenium Engineers ameshukuru na kuipongeza REA kwa kuweza kuwawezesha wawekezaji mbalimbali wakiwamo wao hali iliyowawezesha kuongeza thamani ya soko la dagaa.

 

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top