Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme
Frank A. Mugogo 250

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Hayo yamebainishwa na Msimamizi wa miradi ya REA Mkoani Mtwara, Mhandisi Daniel Mwandupe Oktoba 18, 2025 Wilayani Newala mkoani humo wakati wa kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi kuunganishiwa umeme na kuutumia kujiletea maendeleo.

“Kwa Mkoa wa Mtwara hadi sasa tunaendelea kutekeleza miradi mikubwa miwili yenye thamani ya shilingi bilioni 73.5 ya kusambaza umeme katika vitongoji 611 kati ya vitongoji 1,067 vilivyosalia,” alibainisha Mhandisi Mwandupe.

Akizungumzia mradi kusambaza umeme katika Wilaya hiyo ya Newala, Mhandisi Mwandupe alisema jumla ya vitongoji 39 vitafikishiwa umeme kupitia Mradi wa ujazilizi 2C kwa gharama ya takribani shilingi bilioni 4.7.

“Leo tupo hapa Newala tunatekeleza mradi wa ujazilizi unaotekelezwa na Mkandarasi Mzawa Kampuni ya Sengerema ambaye pia anatekeleza mradi katika wilaya zingine Mkoani Mtwara kwa gharama ya shilingi bilioni 56 na anatekeleza katika vitongoji 461 ndani ya Wilaya za Mtwara, Masasi, Nanyumbu, Tandahimba na Newala,” alisema Mha. Mwandupe.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi kutoka REA, Jaina Msuya alitoa wito kwa wananchi waliofikiwa na mradi kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa umeme ili kujiletea maenedeleo.

“Miradi ya umeme inakuja na fursa nyingi kuanzia hatua za awali za utekelezaji wa mradi hadi mradi unapokamilika kwani mkandarasi atapangoisha nyumba zetu, atafanya manunuzi mbalimbali, atatoa ajira; umeme unaweza kubadilisha maisha yenu, miradi ya umeme ni miradi ya kuwezesha wananchi kiuchumi,” alisisitiza Msuya.

Aliwasisitiza wananchi kuhakikisha wanatunza na kulinda miundombinu ya umeme hasa ikizingatiwa kuwa Serikali imetumia fedha nyingi katika ujenzi wa miradi hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wa Kitongoji cha Amkeni Wilayani Newala, waliipongeza Serikali kwa kufikisha umeme na waliahidi kuwa walinzi wa miundombinu na wataendelea kuhamasishana kuunganisha umeme ili kubadilisha maisha yao.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Amkeni, Sharifu Said alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza kwa kuwafikishia umeme wananchi wa kitongoji cha Amkeni.

Alisema kufika kwa umeme katika kitongoji hicho kutaleta maendeleo kwani wananchi wataanzisha viwanda vidogovidogo na fursa nyingine za kiuchumi zitaibuliwa na hivyo kupanua wigo wa ajira hususan kwa vijana katika kitongoji hicho.

Naye mkazi wa kitongoji cha Amkeni, Dativa Raimond ambaye ni mjasiriamali wa kuuza vinywaji alipongeza uwepo wa mradi huo ambao alisema umemuwezesha kuunganisha umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 pekee na alisema kuwa anatarajia kupitia umeme utamuwezesha kuongeza mauzo kwani ataanza kuuza vinywaji baridi tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top