Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu
Frank A. Mugogo 646

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Akizungumza na Wanahabari, Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka REA, Bi. Jaina Msuya amesema lengo la uhamasishaji huo ni kuongeza hamasa ya kujiunga na huduma ya umeme pamoja na kuongeza uelewa wa faida za matumizi ya nishati ya umeme ili Wananchi wa vijijini wabadili maisha yao kiuchumi na kijamii katika vitongoji vyao.

“Kujiunga na huduma ya umeme wakati mkandarasi akiwa yupo kwenye eneo la Mradi, ni nafuu kwa kuwa Mwananchi atalipia shilingi 27,000 kama gharama ya kujiunga na huduma hiyo ingawa kuna gharama ya kufanya ‘wiring’ na kama Mwananchi atakuwa hana fedha ya kufanya hivyo basi anaweza kununua kifaa maalum kinachitwa *Umeme Tayari* (UMETA) kwa gharama ya shilingi 36,000 tu,” amesema Bi. Jaina.

Kwa upande wake Mhandisi wa Miradi ya Umeme Vijijini mkoani Simiyu, Deusdedit Msanze amesema, uhamasishaji ni muhimu kwa sababu unawakumbusha Wananchi kujiunga na huduma ya umeme ndani ya muda mkandarasi anapokuwa bado yupo kwenye maeneo ya Miradi na kuchelewa kujiunga kunaongeza gharama kwa Wananchi.

Akiwahamasisha Wananchi wa Kitongoji cha Mwamahe, kijiji cha Ikinabushu, kilichopo katika Halmashauri ya wilaya ya Bariadi ambapo mkandarasi, kampuni ya Jiangsu Etern Co., Ltd kutoka China ameshakamilisha ujenzi wa miundombinu na Mradi utafungwa na kukabidhiwa kwa TANESCO, tarehe 15 Novemba, 2025 ambapo katika Wananchi 43 wanaostahili kujiunga na huduma ya umeme ni Wananchi saba (7) tu ndiyo waliojiunga na huduma hiyo.

Baada ya uhamasishaji huo Wananchi 20 walijaza fomu ya maombi ya kujiunga na huduma ya umeme ambapo zoezi hilo liliongozwa na Afisa Uhusiano na Wateja kutoka TANESCO mkoa wa Simiyu, Bwana Amon Bidebuye.

Bwana Amon amesema kila Mwananchi mwenye sifa ya kujiunga na huduma ya umeme anaweza kujaza fomu ya maombi kupitia simu ya aina yoyote (Simu Janja au Kiswaswadu) ili kuomba kuunganishwa na huduma ya umeme kwa kupiga *152*00# na baada ya hapo wanatakiwa wafuate maelekezo ambayo ni rahisi.

“Nitoe wito kwa Wananchi, ukitaka kuomba kujiunga na huduma ya umeme, haulazimiki kwenda ofisi ya TANESCO wilayani au mkoani, unaweza kuomba kujiunga kwa kutumia simu yako ya kiganjani na utatakiwa uwe na namba ya NIDA au na Kitambulisho cha NIDA.” amesisitiza Bwana Amon.

Zoezi la uhamaishaji linaendelea katika wilaya ya Itilima na Meatu na Maswa mkoani humo kwa kupitia mikutano kwa Wananchi pamoja na uhamasishaji wa nyumba kwa nyumba.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top