Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI
Admin.Frank Mugogo 9687

BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI

1. Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini leo tarehe 08 Juni 2019 imekutana wa Wakandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I katika Ukumbi wa Hazina, Dodoma kujadili changamoto mbalimbali zinazoweza kuchelewesha utekelezaji wa Mradi. Pia Menejimenti ya REA ilishiriki mkutano huo. Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I unagharimu Shilingi Trilioni 1.2, ukiwa ni mradi mkubwa kusini mwa jangwa la Sahara ambapo vijiji 3,559 vitaunganishwa na huduma ya nishati ya umeme nchi nzima.

2. Bodi ya Wakurugenzi ilitaka kujua mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa Mradi huo pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi kama vile nguzo, nyaya, transfoma, mita na vifaa vingine. Mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa watengenezaji vifaa hivyo yanaleta tija katika kuharakisha utekelezaji wa mradi.

3. Wakandarasi walieleza baadhi ya changamoto kuhusu kuchelewa kupata vifaa wanavyoagiza kutoka kwa watengenezaji. Bodi ilielezwa na watengenezaji wa vifaa hivyo kuwa wanavyo vya kutosha na watarekebisha kasoro zozote zilizojitokeza ili kuwawezesha Wakandarasi kukamilisha utekelezaji wa Mradi kwa wakati.

4. Bodi, baada ya kuwasikiliza Wakandarasi pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi, ilieleza kuwa changamoto zilizoelezwa ziko ndani ya uwezo wa kutatuliwa. Changamoto kubwa iliyoonekana ilikuwa ni uelewa wa baadhi ya taratibu ikiwemo bondi inayowekwa na Benki.

5. Mkutano ulisisitiza kuwa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I utakamilika ifikapo Desemba, 2019 na Wakandarasi atakayechelewesha Mradi kwa mujibu wa Mkataba hawatavumiliwa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top