Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA
Admin.Frank Mugogo 4569

BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) haijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida unayotekelezwa na Kampuni ya Emerc and Dynamic Engineering.

Mwenyekiti wa REB, Wakili Julius Kalolo alionesha wasiwasi huo kwa mkandarasi huyo kushindwa kukamilisha kazi hiyo wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku mbili, tarehe 26 hadi 27 Agosti 2020 ya kukagua utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika wilaya za SingidaVijijini, Iramba na Mkalama.

“Tumeona kwa kiasi fulani ametimiza maukumu yake, lakini bado yupo chini ya matarajio kwa sababu maeneo mengi hayajajengwa miundombinu ya umeme mkubwa, hata miundombinu ya umeme mdogo kwa ajili ya kuingiza majumbani hajakamilika” alisema.

Kutokana na kusuasua kwa mkandarasi huyo, Bodi ilimuagiza aongeze magenge ya kazi ili aweze kukamilisha mradi huo ifikapo tarehe 10/09/2020. Hata hivyo, Wakili Kalolo alisema mkandarasi amepewa siku tatu kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti, 2020 ambapo kama hatajirekebisha kwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi, atapunguziwa wigo wa mradi wake ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati uliopangwa.

“Atakuwa katika uangalizi wa siku tatu kama hataonesha mabadiliko atapunguziwa kazi ili asicheleweshe wananchi kupata huduma ya nishati ya umeme” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu amemtaka mkandarasi kuzingatia maelekezo aliyopewa na Bodi na kutahadharisha kuwa ndani ya siku tatu kama hataonesha mabadiliko ya utendaji wake wa kazi atapunguziwa baadhi ya maeneo.

“Tumempa tahadhari baada ya siku tatu baadhi ya maeneo ambayo atakuwa hajaanza kazi TANESCO wataingia na mafundi wao kukamilisha ili wananchi waweze kuwashiwa umeme,” alisema.

Mhandisi Olotu alimuagiza mkandarasi kutumia nguvu kazi ya vijana wa vijiji ambavyo viko katika wigo wa mradi katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu kama vile kufyeka vichaka, kuchimba mashimo na kubeba nguzo.

Akizungumza kwa niaba ya mkandarasi, Mhandisi anayesimamia mradi huo, James Kinyila alisema kuwa wamepanga magenge ya kutosha ili kukamilisha kazi hiyo kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top