Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele
Frank A. Mugogo 66

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Wametoa pongezi hizo kijijini hapo Agosti 12, 2025 wakati wa zoezi la usambazaji wa majiko ya gesi (LPG) ya kilo sita na vichomeo vyake kwa bei ya ruzuku ya shilingi 19,500 kwa kila jiko.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutuletea majiko haya yanakwenda kurahisisha maisha yetu, majiko haya pia ni mkombozi wa mazingira naamini ukataji wa miti unakwenda kupungua," alisema Davis Majaliwa Mkazi wa Usevya.

Kwa upande wake Christina Sindano mkazi wa Kijiji cha Usevya alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele katika kampeni hiyo ambayo alisema inanufaisha wananchi wake hususan kina mama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Usevya, Focus Kapongwa alisema wananchi kijijini hapo wamekuwa na mazoea ya kukata miti kwa ajili ya kuni na mkaa lakini kufika kwa mradi kutapunguza ukataji holela wa miti.

"Tunashukuru kwa hii huduma, tumepata shida sana kwenye ununuzi wa mkaa kwani sasa hivi mkaa ni bei ghali na haya majiko yatatusaidia kupunguza gharama ya maisha," alisema Kapongwa.

Akizungumza kuhusu mradi, Mtaalam wa Jinsia na Nishati wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt.Joseph Sambali alisema mradi huo kwa Mkoa wa Katavi unatekelezwa kwa kushirikiana na Kampuni ya Taifa Gas Limited ambapo jumla ya majiko 3,255 ya gesi (LPG) ya kilo sita ikiwa na mafiga viwashia vyake yatasambazwa kwa bei ya ruzuku katika kila wilaya ya Mkoa wa Katavi. 

"Majiko haya yanauzwa kwa bei ya ruzuku gaharama zingine zimebebwa na Serikali lengo ni kuhakikisha nishati safi ya kupikia inapatikana kwa gharama nafuu ambayo kila mwananchi anamudu," alisema Dkt. Sambali.

Alisisitiza kuwa kila mwananchi anapaswa kuwa na kitambulisho cha Taifa (NIDA) ili kuepuka watu kujirudia kwani dhamira ni kufikiwa kwa kila mwananchi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Mlele, Yahaya Mbulu alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ikiwemo ya nishati safi ya kupikia.

"Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele kwenye Niishati Safi ya kupikia; inakadiriwa kuwa takribani watu 31,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na matumizi ya nishati isiyo salama," alibainisha Mbulu.

Alitoa wito kwa wananchi kuacha kuharibu mazingira kwa kukata miti badala yake wachangamkie fursa hiyo ya majiko ya gesi kwa bei ya ruzuku.


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top