Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala
Frank A. Mugogo 98

REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala

Wakala wa Nishati Vijijini unahamasisha wananchi kote nchini kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo Mkaa mbadala ambao umeelezwa kuwa na gharama nafuu na ni salama kwa afya ya mtumiaji na mazingira.

Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala, Mhandisi Advera Mwijage kutoka REA ametoa wito huo Mei 31, 2025 alipotembelea na kukagua uzalishaji wa mkaa mbadala unaotokana na mabaki ya makaa ya mawe katika kiwanda cha Rafiki Briquettes kinachomilikiwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kilichopo Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani.

"Watanzania tusiogope mabadiliko katika matumizi ya nishati safi mbalimbali za kupikia. Mkaa unaozalishwa kutokana na mabaki ya makaa ya mawe ni salama kiafya,safi na nafuu sana katika matumizi. Katika ziara hii nimetembelea hapa nimejiridhisha pasi na shaka mkaa huu ni salama kutokana na teknolojia inayotumika katika utengenezaji," alisisitiza Mhandisi Advera.

Alisema REA inatekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia na miongoni mwa majukumu iliyopewa ni kuhamasisha na kuwezesha uzalishaji, usambazaji wa bidhaa za nishati safi ya kupikia ili kila mwananchi afikiwe na amudu gharama zake.

Alisema ametembelea kiwanda hicho ili kushuhudia hali ya uendeshaji wake, kujionea uzalishaji wa mkaa mbadala ili kuwaondolea baadhi ya wananchi dhana iliyojengeka miongoni mwao ya kwamba mkaa huo si salama na pia kuona namna ambavyo serikali kupitia REA itaendelea kuwezesha uzalishaji wa mkaa huo.

"Hapa ninavyozungumza tayari tumepokea maombi kutoka STAMICO ya kuwawezesha kununua mitambo mingine ili waweze kutanua wigo wa uzalishaji, nimeridhishwa na kazi inayofanyika na sisi REA tunaahidi kuendeleza ushirikiano ili kufikia lengo na dhamira ya Serikali inayoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan," alifafanua Mha. Advera.

Alishauri STAMICO kushirikiana na vyombo vya habari na makundi mbalimbali katika jamii katika kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mkaa huo ili kuondoa dhana hiyo mbaya miongoni mwa jamii.

Akizungumzia malengo na hali ya uzalishaji, Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO, Deusdedith Magala alisema kiwanda hicho kinao uwezo wa kuzalisha kiasi cha tani 20 kwa saa na kwamba mbali na kiwanda hicho cha Kisarawe, STAMICO inamiliki viwanda vingine viwili kimojawapo kikiwa Dar es Salaam eneo la Tirdo na kingine Kiwira kulipo na malighafi hiyo ya makaa ya mawe.

"Lengo letu ni kuwa na viwanda 21 Tanzania Bara ili kurahisisha ufikishaji wa bidhaa kwa wananchi kwa gharama ambayo kila mwananchi anamudu, kwa sasa kilo moja ya mkaa kwa bei ya rejareja tunauza kwa shilingi 1,000 na kwa bei ya jumla ni shilingi 800," alisema Magala.

Alisema viwanda viwili viko mbioni kukamilika kimoja kinajengwa Mkoani Dodoma na kingine kinajengwa Mkoani Tabora kwa lengo la kupunguza ukataji ovyo wa miti unaofanywa na wakulima wa tumbaku mkoni humo wakati wa kukausha zao hilo," alisema Magala.

Naye Mhandisi Muendeshaji wa kiwanda hicho, Goodluck Mhagama alisema mkaa huo ni rahisi ikilinganishwa na mkaa wa miti kwani kilo moja inaweza kutumika kupikia kwa zaidi ya Saa 4 bila kupunguza ukali wake.

"Kilo moja ya mkaa huu unaweza kupikia maharagwe, nyama, wali ama kusonga ugali na hata kuchemsha maji bila kuongeza mkaa mwingine, wewe kazi yako ni kubadilisha tu sufuria," alsema Mhandisi Mhagama.

Alisema uandaaji wa mkaa huo umezingatia vigezo vyote muhimu na kwamba mkaa huo ni salama na hauna madhara yoyote kwa mtumiaji ama kwa mazingira na kwamba umethibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top