Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 11091

MAFUNZO YA KUENDELEZA TEKNOLOJIA ZA NISHATI JADIDIFU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2014/2015 umepanga kutoa mafunzo ya hadi wiki mbili kwa wajasiriamali wanaoendeleza vyanzo vya umeme unaofuliwa kutokana na nishati jadidifu. Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo mafundi na waendelezaji wa teknolojia za nishati bora waliopo maeneo ya vijijini ili waweze kutoa huduma bora.

Wakala unakaribisha maombi kutoka kwa mafundi na waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini katika teknolojia zifuatazo:

1. Nishati itokanayo na maporomoko madogo ya maji

2. Nishati itokanayo na tungamotaka (biogas & biomas)

3. Nishati itokanayo na upepo

4. Utayarishaji wa mpango biashara

5. Nishati itokanayo na mionzi ya jua

Sifa za Mwombaji

Waombaji wawe na elimu ya Kidato cha Nne (wenye vyeti vya ufundi VETA Daraja la 1 watapewa kipaumbele)

Maombi yote yatumwe yakiwa na taarifa zifuatazo:

1. Jina, anwani, namba ya simu ya atakayehudhuria mafunzo, kazi anayofanya, uzoefu wake na vivuli v ya vyeti vya elimu aliyonayo.

2. Iwapo maombi yatapitia katika taasisi/mradi wa nishati; Jina kamili la taasisi/mradi wa mwombaji, Jina la atakayehudhuria mafunzo, nakala ya vyeti vya elimu aliyonayo, anwani na namba ya simu ya taasisi ikiwa ni pamoja na maelezo mafupi kuhusu uzalishaji wa chanzo husika, mahali chanzo kilipo, uwezo wake wa kuhudumia jamii au idadi ya wateja wanaotegemea kuunganishwa/kufaidika na huduma hiyo.

Wakala utasimamia na kugharamia mafunzo husika. Mwombaji atatakiwa kugharamia usafiri wa kwenda na kurudi katika mafunzo.

Maombi yatumwe kwenye anuani ifuatayo kabla ya tarehe 15/08/2014.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S.L.P. 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Parua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print

Documents to download

«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top