Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 11041

MAFUNZO YA KUENDELEZA TEKNOLOJIA ZA NISHATI JADIDIFU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2014/2015 umepanga kutoa mafunzo ya hadi wiki mbili kwa wajasiriamali wanaoendeleza vyanzo vya umeme unaofuliwa kutokana na nishati jadidifu. Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo mafundi na waendelezaji wa teknolojia za nishati bora waliopo maeneo ya vijijini ili waweze kutoa huduma bora.

Wakala unakaribisha maombi kutoka kwa mafundi na waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini katika teknolojia zifuatazo:

1. Nishati itokanayo na maporomoko madogo ya maji

2. Nishati itokanayo na tungamotaka (biogas & biomas)

3. Nishati itokanayo na upepo

4. Utayarishaji wa mpango biashara

5. Nishati itokanayo na mionzi ya jua

Sifa za Mwombaji

Waombaji wawe na elimu ya Kidato cha Nne (wenye vyeti vya ufundi VETA Daraja la 1 watapewa kipaumbele)

Maombi yote yatumwe yakiwa na taarifa zifuatazo:

1. Jina, anwani, namba ya simu ya atakayehudhuria mafunzo, kazi anayofanya, uzoefu wake na vivuli v ya vyeti vya elimu aliyonayo.

2. Iwapo maombi yatapitia katika taasisi/mradi wa nishati; Jina kamili la taasisi/mradi wa mwombaji, Jina la atakayehudhuria mafunzo, nakala ya vyeti vya elimu aliyonayo, anwani na namba ya simu ya taasisi ikiwa ni pamoja na maelezo mafupi kuhusu uzalishaji wa chanzo husika, mahali chanzo kilipo, uwezo wake wa kuhudumia jamii au idadi ya wateja wanaotegemea kuunganishwa/kufaidika na huduma hiyo.

Wakala utasimamia na kugharamia mafunzo husika. Mwombaji atatakiwa kugharamia usafiri wa kwenda na kurudi katika mafunzo.

Maombi yatumwe kwenye anuani ifuatayo kabla ya tarehe 15/08/2014.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S.L.P. 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Parua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print

Documents to download

«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top