Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 11093

MAFUNZO YA KUENDELEZA TEKNOLOJIA ZA NISHATI JADIDIFU

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2014/2015 umepanga kutoa mafunzo ya hadi wiki mbili kwa wajasiriamali wanaoendeleza vyanzo vya umeme unaofuliwa kutokana na nishati jadidifu. Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo mafundi na waendelezaji wa teknolojia za nishati bora waliopo maeneo ya vijijini ili waweze kutoa huduma bora.

Wakala unakaribisha maombi kutoka kwa mafundi na waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini katika teknolojia zifuatazo:

1. Nishati itokanayo na maporomoko madogo ya maji

2. Nishati itokanayo na tungamotaka (biogas & biomas)

3. Nishati itokanayo na upepo

4. Utayarishaji wa mpango biashara

5. Nishati itokanayo na mionzi ya jua

Sifa za Mwombaji

Waombaji wawe na elimu ya Kidato cha Nne (wenye vyeti vya ufundi VETA Daraja la 1 watapewa kipaumbele)

Maombi yote yatumwe yakiwa na taarifa zifuatazo:

1. Jina, anwani, namba ya simu ya atakayehudhuria mafunzo, kazi anayofanya, uzoefu wake na vivuli v ya vyeti vya elimu aliyonayo.

2. Iwapo maombi yatapitia katika taasisi/mradi wa nishati; Jina kamili la taasisi/mradi wa mwombaji, Jina la atakayehudhuria mafunzo, nakala ya vyeti vya elimu aliyonayo, anwani na namba ya simu ya taasisi ikiwa ni pamoja na maelezo mafupi kuhusu uzalishaji wa chanzo husika, mahali chanzo kilipo, uwezo wake wa kuhudumia jamii au idadi ya wateja wanaotegemea kuunganishwa/kufaidika na huduma hiyo.

Wakala utasimamia na kugharamia mafunzo husika. Mwombaji atatakiwa kugharamia usafiri wa kwenda na kurudi katika mafunzo.

Maombi yatumwe kwenye anuani ifuatayo kabla ya tarehe 15/08/2014.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S.L.P. 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Parua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print

Documents to download

«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top