Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo
Frank A. Mugogo 349

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.
 
Pongezi hizo zimetolewa leo Julai 1, 2025 na Mjumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Lucas Malunde wakati akimwakilishi Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu katika hafla ya kugawa mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na jiko la gesi la sahani mbili kwa Watumishi wa Magereza Mkoa wa Simiyu.
 
"Mei 8, 2024, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alizindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia. Toka kuzinduliwa kwa mkakati huo, Serikali imefanya juhudi mbalimbali kuhakikisha Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ili kuokoa mazingira pamoja na vifo vilivyokuwa vinatokana na matumizi ya nishati isiyokuwa safi na salama ya kupikia.
 
Mhe. Rais ameweza kutoa fedha zilizowezesha magereza zote nchini kuachana na matumizi ya kuni na kuanza kutumia nishati safi ya kupikia. Na leo tuko hapa kugawa mitungi ya gesi pamoja na majiko yake kwa Watumishi wa Magereza. Zote hizi zikiwa ni juhudi za Mhe. Rais kuhakikisha Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unatekelezwa kwa vitendo," amesema Mjumbe huyo wa Bodi.
 
Awali akitoa taarifa kuhusu mradi huo, Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Wawekezaji Miradi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema kuwa jumla ya mitungi ya gesi ya Kilogramu 15 na majiko ya gesi ya sahani mbili 330 itagaiwa kwa Watumishi wa Magereza Mkoa wa Simiyu.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Simiyu, SACP Lugano Msomba ameishukuru Serikali kupitia REA kwa kuwawezesha Watumishi wa Magereza kupata nishati safi ya kupikia na kuahidi kuwa watakuwa mabalozi kwa wengine katika kampeni hiyo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top