Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Ahamasisha Wananchi Kutumia Nishati Safi ya Kupikia
Aodax K. Nshala 300

Mkurugenzi Mkuu REA Ahamasisha Wananchi Kutumia Nishati Safi ya Kupikia

Serikali Imetoa Ruzuku Katika Mitungi ya Gesi (LPG) Na Majiko Banifu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewaasa wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuokoa gharama na muda, kulinda mazingira na afya zao hasa ikizingatiwa kuwa teknolojia sasa imeboreshwa na gharama yake ni nafuu ikilinganishwa na nishati zingine. 

Mhandisi Saidy ametoa rai hiyo Agosti 8, 2024 mbele ya wananchi waliotembelea Banda la REA katika Maonesho ya Siku Kuu ya Wakulima (Nane Nane), Nzuguni Jijini Dodoma. 

"Tunaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia kwani ni salama, rafiki na gharama yake ni nafuu kwani teknolojia sasa imeboreshwa," amesema Mhandisi Saidy. 

 Mhandisi Saidy amesema ipo dhana ambayo imejengeka katika jamii kuwa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ni ghali na si salama na pia chakula kinachopikwa kutokana nayo hakina ladha suala ambalo alisisitiza halina kweli. 

"Ninawathibitishia Nishati Safi ya Kupikia ni salama kuliko nishati zingine tulizozizoea, niwatoe wasiwasi katika hili na tunaendelea kutoa elimu kuhusu usalama na umuhimu wa nishati hii bora," amesema Mhandisi Saidy.

Akizungumzia upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia kwa wote, amesema Serikali imetoa ruzuku katika usambazaji wa Mitungi ya Gesi (LPG) na Majiko Banifu ili kuvutia wawekezaji wengi na pia kumuwezesha kila mwananchi aweze kumudu gharama zake. 

"Serikali imekuja na mfumo wa kumrahisishia kila mwananchi hususan yule mwenye kipato cha chini kumudu gharama ya Nishati Safi ya Kupikia kokote aliko ili aachane na matumizi ya nishati nyingine," amefafanua Mhandisi Saidy. 

Amesema Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipatia REA jukumu la kuhakikisha inasimamia vyema utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ili kufikia 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia. 

"Tunamshukuru Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuamini na kutupatia jukumu hilo kubwa na tayari kwa kushirikiana na wadau tumeanza utekelezaji wake na tunakwenda vizuri," amefafanua Mhandisi Saidy. 

Amesema hatua inayoendelea sasa ni kuibua na kuwawezesha wazalishaji wengi wa vifaa vya Nishati Safi ya Kupikia ili kuongeza umahiri sambamba na kuwawezesha kutengeneza bidhaa nyingi kwa gharama nafuu na kwa ubora wa kimataifa," amesema. 

Amesema kwa kufanya hivyo kutakuwa na ongezeko la matumizi ya nishati safi ya kupikia, ongezeko la ajira na hivyo kukuwa kwa uchumi.
 

Imetolewa na:
Mohamed M. Seif
msaif@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top