Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Aipongeza REA
Aodax K. Nshala 113

Rais Samia Aipongeza REA

Atembelea Kitua Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme cha Ifakara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi nzuri wanazofanya.

Mhe. Rais ametoa pongezi hizo leo Agosti 4 wilayani Kilombero, Mkoa wa Morogoro alipotembelea Kituo cha Kupokea na Kupoza umeme cha Ifakara kilichojengwa na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya kilichotatua changamoto ya muda mrefu ya umeme wa uhakika katika Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Ifakara.

Awali akitoa maelezo kuhusu mradi huo, Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia kwa kuridhia kupitia Wizara ya Nishati kujenga vituo 75 vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme ikiwa ni jitihada zake za kuhakikisha wananchi katika maeneo yote wanapata umeme wa uhakika.

"Kabla ya mwaka 2021 nchi ilikuwa ina vituo 61 tu vya kupokea na kupoza umeme, tunakushukuru sana Mhe. Rais kwa kuridhia ujenzi wa vituo vingine vipya 75." Amesema Mhe. Kapinga

Mhe. Naibu Waziri Kapinga amesema kuwa, tayari vituo nane vimejengwa na kuanza kazi huku vituo sita vikifikia asilimia 97.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema kituo cha Ifakara kimejengwa kutokana na uhitaji mkubwa wa umeme wilayani Ifakara, Malinyi na Ulanga na hii pia inatokana na shughuli kubwa za kilimo na uchimbaji madini.

Mhandisi Hassan ameongeza kuwa, kabla ya ujenzi kituo cha Ifakara umeme kwa mwezi ulikuwa ukikatika mara 18 ambapo hivi sasa ikitokea umeme umekatika basi ni mara moja.

Ameongeza kuwa gharama ya ujenzi wa kituo hicho ilikuwa ni shilingi bilioni 24.5 ambapo serikali imechangia gharama hizo pamoja na wadau wa maendeleo ambao ni Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) na kukamilika kwa kituo hicho haujasaidia tuu kuongeza thamani ya mazao bali pia umesaidia kuboresha huduma za kijamii kama afya kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika katika hospitali na zahanati.
 

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top