Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA itaendelea kufanya tafiti za ufanisi wa bidhaa za nishati safi za kupikia
Frank A. Mugogo 27

REA itaendelea kufanya tafiti za ufanisi wa bidhaa za nishati safi za kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala utaendelea kufanya tafiti za bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ili kubaini ufanisi wa teknolojia zinazosambazwa kwa wananchi.

Mhandisi Saidy amesema hayo Agosti 23, 2024 alipotembelea Banda la Wakala katika Tamasha la Kizimkazi eneo la Kizimkazi Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

"Tutaendelea kufanya utafiti wa bidhaa mbalimbali za Nishati Safi za Kupikia ili kutimiza dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Nishati Safi ya Kupikia kwa wote inapatikana kwa gharama nafuu na yenye ufanisi," amesema.

Amesema dhamira ni kuwa na teknolojia sahihi, rafiki na yenye gharama nafuu ili kumuwezesha na kumrahisishia kila Mwananchi kuwa na bidhaa bora.

"Tutahakikisha lengo la Serikali kupitia Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 la kufikisha asilimia 80 ya wananchi wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034 linafikiwa," amesema.

Mhandisi Saidy vilevile alitembelea mabanda ya Wadau wanaojihusisha na uandaaji, uuzaji na usambazaji wa Nishati Safi ya Kupikia na kujadiliana masuala mbalimbali hususan namna bora ya kuendelea kuboresha bidhaa zao ili kuleta tija inayokusudiwa.

Awali kabla ya kutembelea  Maonesho ya Kizimkazi, Mhandisi Saidy alishiriki Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia lililoandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF) na Benki ya Uwekezaji ya Tanzania (TIB) kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Taasisi zake ikiwemo REA ambapo Wakala ulipata fursa ya kuelezea suala la Upatikanaji wa Fedha katika kuendeleza Nishati Safi ya Kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
26
REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Read more
27
Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewaasa wananchi kutunza mazingira na kulinda miundombinu pamoja na vyanzo vya maji ili kuendelea kupata huduma ya umeme pamoja na kuwa na miradi endelevu ya kufua umeme.

Read more
282930311
2345678
9101112
EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

The Government of Tanzania through the Rural Energy Agency (REA) in collaboration with Tanzania Prisons Services (TPS) in response to attainment of sustainable development goals, has opened a   financing   window to support distribution of 15,920 units of 15kg LPG Starter Packs to earmarked Staffs in all Tanzania Prisons. This is part of the Clean Cooking Packages that the parties have agreed to cooperate inorder to enable these institutions to stop using environmentally and healthily harmful cooking solutions.

Read more
131415
16171819202122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top