Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MPANGO KABAMBE UPELEKAJI NISHATI VIJIJINI WABAINISHWA
Admin.Frank Mugogo 974

MPANGO KABAMBE UPELEKAJI NISHATI VIJIJINI WABAINISHWA

Na Veronica Simba - Kigoma

Imeelezwa kuwa Mpango Kabambe wa Kupeleka Nishati Vijijini umelenga kuwanufaisha wananchi kupitia usambazaji umeme pamoja na nishati bora ya kupikia.

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki wakati wa ziara ya viongozi wakuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) mkoani Kigoma.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Saidy, walisema kuwa Mpango huo unahusisha nishati za aina mbalimbali, siyo umeme peke yake.

Wakili Kalolo alisema kuwa, ni jukumu la REA kuhakikisha wananchi waishio vijijini wanapata nishati safi na zenye gharama nafuu ili ziwasaidie kuboresha maisha yao, hivyo Wakala umejiwekea mikakati ya kuhakikisha jukumu hilo linatekelezwa ipasavyo.

Akifafanua, alisema kuwa REA imefanikiwa kwa kiasi kikubwa na inaendelea kufanya vema katika utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, hivyo hakuna shaka katika utekelezaji wa miradi ya aina nyingine za nishati zilizofanyiwa tafiti, utakuwa wenye ufanisi pia.

Akitoa mfano, alisema kuwa tafiti zinaonesha eneo jingine muhimu linalopaswa kupewa kipaumbele ni katika nishati ya kupikia ambapo asilimia kubwa ya waathirika ni wanawake, ambao kutokana na matumizi ya kuni, wamekuwa wakisumbuliwa na magonjwa ya macho na kifua.

Alisema, ni kwa sababu hiyo, Wakala umedhamiria kuondoa adha hiyo katika jamii hususani wanawake waishio vijijini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu akidadavua zaidi kuhusu Mpango huo kabambe, alieleza kuwa umejikita katika sehemu mbili kubwa ambazo ni usambazaji umeme pamoja na nishati ya kupikia.

Alieleza zaidi kuwa, hivi sasa, Wakala unaongeza nguvu zaidi katika nishati ya kupikia ili kuhakikisha kwamba wananchi hususan wa vijijini, wanatumia nishati bora kwa shughuli za kupikia na kupunguza au kuachana kabisa na matumizi ya kuni na mkaa ambao upatikanaji wake ni mgumu, aghali na siyo rafiki kwa mazingira.

Mhandisi Saidy alisema REA imefanya tafiti kadhaa za majaribio kuhusu nishati ya kupikia mathalani mradi wa kutumia tungamotaka, ambapo mifumo husika ilipelekwa katika maeneo 725 yaliyopo sehemu mbalimbali nchini.

Aidha, aliongeza kuwa, Wakala umeshirikiana na kampuni za usambazaji gesi kufanya tafiti kuhusu uwezekano wa kuhakikisha nishati ya gesi inafikishwa katika maeneo ya vijijini kwa gharama nafuu ili wananchi waweze kuitumia kwa shughuli za kupikia.

Katika hatua nyingine, viongozi hao waliwahakikishia Wakuu wa Wilaya za Kibondo na Kakonko, ambao walikutana nao kwa nyakati tofauti, kuwa maeneo yote ya kimkakati, hasa yanayohusisha masuala ya usalama yatapelekewa huduma ya umeme ili kuwezesha shughuli hizo kufanyika kwa ufanisi.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Evance Malassa na Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanali Aggrey Magwaza, kwa nyakati tofauti waliomba maeneo ya mpakani ambayo hayajafikiwa na huduma ya umeme, yapewe kipaumbele katika kufikishiwa nishati hiyo ili kuimarisha shughuli za kiusalama.

Pia, Wakuu hao wa Wilaya walipongeza jitihada ambazo zimekuwa zikifanywa na Wakala wa Nishati Vijijini katika kusambaza umeme vijijini kupitia miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.

Katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu pia walikagua miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kukutana na wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo ambapo walijadili changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

Kupitia kikao hicho, viongozi hao waliipatia ufumbuzi changamoto ya upatikanaji vifaa iliyokuwa ikimkabili Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza, Kampuni Tanzu ya TANESCO (ETDCO) katika wilaya za Kakonko na Kibondo.

“Utekelezaji ulikuwa nyuma kidogo kutokana na changamoto ya vifaa. Tumetatua changamoto hiyo na tumemwelekeza Mkandarasi ndani ya miezi mitatu awe amekamilisha mradi huu,” alisema Mkurugenzi Mkuu.

Aidha, Mkandarasi anayetekeleza Mradi huo katika wilaya za Buhigwe, Kasulu, Kigoma Vijijini na Uvinza, Kampuni ya M/s CCCE Etern Consortium alielekezwa kuongeza nguvu ili akamilishe kazi hiyo kwa wakati uliopangwa ambao ni mwishoni mwa mwezi huu wa Desemba, 2021.

Miradi mingine inayotekelezwa mkoani Kigoma ni pamoja na REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotarajiwa kuanza hivi karibuni pamoja na Mradi wa Ujazilizi unaolenga kufikisha umeme katika maeneo yaliyopitiwa na miundombinu ya nishati hiyo lakini umeme haujashushwa.

Katika ziara hiyo, viongozi hao wa REA waliambatana na wataalamu mbalimbali kutoka Wakala hiyo pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top