Naibu Waziri Wizara ya Nishati, Mhe. Salome Makamba ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii maeneo ya vijijini kupitia Usambazaji wa Umeme na Teknolojia zilizoboreshwa za Nishati Safi ya Kupikia.
Ametoa pongezi hizo Aprili 22, 2026 alipofanya ziara kwenye banda la REA katika Maonesho ya Wiki ya Nishati 2026 na kuzungumza na watendaji.
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni miongoni mwa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ambayo inashiriki katika Maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu na taarifa za utekelezaji wa Miradi ya Usambazaji wa Nishati kwa Wabunge na wageni wa Bunge wanaotembelea Banda la Maonesho.