Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Imeleta Mageuzi Sekta Ya Nishati
Mohamed Saif 173

REA Imeleta Mageuzi Sekta Ya Nishati

Mkurugenzi Mkuu REA apongezwa

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii maeneo ya Vijijini kupitia miradi ya Usambazaji Umeme na uhamasishaji na uwezeshaji wa Teknolojia zilizoboreshwa za Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi kote nchini.

Hayo yameelezwa Aprili 23, 2026 na Mbunge wa Sikonge ambaye pia aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhe. Mha. Amos Maganga.

"Ninawapongeza sana REA, mnafanya kazi kubwa, miradi mliyotekeleza kote nchini imechagiza ukuaji wa uchumi Vijijini lakini pia imeboresha huduma za Jamii katika maeneo hayo," amebainisha Maganga.

Amesema kwa sasa hakuna tofauti kati ya vijiji na miji kwani kupitia miradi iliyotekelezwa na REA huduma muhimu ikiwemo za afya na elimu kote zinapatikana kwa ubora sawa.

Aidha, wakizungumza kwa nyakati tofauti, Wabunge waliotembelea Banda la REA walimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy kwa uongozi wake ambao walisema umeleta chachu kwenye utekelezaji wa miradi.

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top