Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Kuendelea Kuwezesha Waendelezaji wa Miradi ya Nishati Vijijini
Frank A. Mugogo 342

REA Kuendelea Kuwezesha Waendelezaji wa Miradi ya Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) utaendelea kutoa sapoti kwa waendelezaji wa miradi ya kuzalisha na kusambaza umeme kote nchini ili kuwezesha wananchi wengi kufikiwa na huduma bora ya nishati ambayo inachangia kuinua uchumi wa wananchi pamoja na huduma za kijamii.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu amebainisha hayo Mkoani Njombe Juni 17, 2025 kwa Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anthony Mtaka alipofika ofisini kwake kuelezea ziara yake ya kukagua miradi ya kuzalisha na kusambaza umeme mkoani humo.

"Njombe ni moja ya Mkoa ambayo imepokea sapoti kubwa kwenye uendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu," alisema Mhe. Balozi Kingu.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Mtaka alimueleza Mhe. Balozi Kingu namna ambavyo anafarijika kwa sapoti inayotolewa na REA kwenye miradi hiyo na alisema kwa namna mkoa huo ulivyo bado zipo fursa nyingi za kuzalisha umeme kwa maporomoko ya maji ya mito.

"Jiografia ya mkoa huu inaruhusu kuwa na miradi mingi ya kuzalisha umeme na bahati nzuri wananchi wanao mwamko mkubwa katika kubuni na kuanzisha miradi ya kuzalisha umeme," alisema Mhe. Mtaka.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa huo, Dorica Omary aliipongeza Bodi ya Nishati Vijijini (REB) kwa usimamizi mzuri wa miradi inayotekelezwa na kusimamiwa na REA.

"Miongoni mwa miradi ambayo inatupa faraja hapa ni miradi ya REA, kwakweli mnafanya kazi nzuri, suala la umeme hapa tupo vizuri," alipongeza Judica.

Mhe. Balozi Kingu yupo Mkoani Njombe kwa ziara ya siku nne kwa lengo la kutembelea na kukagua uendelezwaji wa miradi mbalimbali inayowezeshwa na REA akiwa ameambatana na Wataalam kutoka Wakala wakiongozwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Nishati Jadidifu na Mbadala, Mhandisi Advera Mwijage.

Mhandisi Mwijage alisema kuwa Mkoa wa Njombe kuna vyanzo saba vya kuzalisha umeme vyenye Jumla ya Megawati 6.8 ambavyo vimefadhiliwa na REA na vimeunganisha wateja zaidi ya elfu tano.

Akizungumzia miradi hiyo, Mhandisi Mwijage alisema mbali na kuongeza kiwango cha uzalishaji wa umeme, miradi hiyo pia ni rafiki wa mazingira kwa kuwa haizalishi hewa ya Ukaa.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top