Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani
National

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani

Utekelezaji wa mradi wa kusambaza gesi asili katika eneo la Kisemvule, wilayani Mkuranga mkoani Pwani, umeendelea kuibua matumaini mapya kwa Wananchi wa eneo hilo ambapo zaidi ya shilingi bilioni 6.8 zimewekezwa katika kusambaza gesi asilia katika maeneo yaliyopitiwa na mkuza wa bomba la gesi asilia.

Mradi huo umejengwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na kufadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeelezwa kuwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuhakikisha ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya Watanzania watakuwa wanatumia nishati safi ya kupikia.

Akizungumza baada ya kutembelea na kukagua Mradi huo; Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, amesema utekelezaji wa Mradi huo unaonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuboresha maisha ya Wananchi na kulinda mazingira.

Amesema Bodi ya Nishati Vijijini inajivunia kuona mwitikio mkubwa wa Wananchi wanaendelea kuhamasika ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake kutumia gesi asili, ambayo ni salama, nafuu na rafiki kwa mazingira.

“Huu ni Mradi wa kimkakati unaotekeleza maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuona Watanzania wengi wanatumia nishati safi, tunapaswa kulinda miundombinu hii kwa kuwa imegharimu fedha nyingi za Serikali,” amesema Balozi Kingu.

Kwa mujibu wa REA, mradi huo wa mfano ulilenga kuhudumia kaya 2,000 huku hadi sasa kaya 530 zikiwa zimefikiwa na huduma hiyo katika eneo la Kisemvule lenye wakazi zaidi ya 64,000 hali inayotoa fursa ya kupanua zaidi wigo wa huduma hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi, Hassan Saidy amesema taasisi hiyo imeiomba TPDC kufanya tathmini katika maeneo yenye idadi kubwa ya watu ambako bomba la gesi limepita ili kuanzisha miradi ya ubia itakayowezesha wananchi wengi zaidi kuunganishwa na huduma hiyo.

Ametaja baadhi ya maeneo yanayopendekezwa kuwa ni Mkuranga Mjini, Ikwiriri na Kilwa Kivinje, akibainisha kuwa hatua hiyo itaharakisha utekelezaji wa Sera ya Nishati Safi nchini.

Naye Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia za Nishati Mbadala kutoka REA, Mhandisi, Advera Mwijage amesema Bodi ya Nishati Vijijini imeagiza kuongeza kasi ya uunganishwaji wa kaya zaidi ili Mradi huo unufaishe Wananchi wengi zaidi kulingana na mahitaji halisi ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Mhandisi, Tumaini Daniel, Meneja Mradi kutoka TPDC amesema Mradi huo umekamilika kwa mafanikio na umeweka msingi mzuri wa upanuzi wa huduma hiyo katika maeneo mengine yenye miundombinu ya bomba la gesi.

Wananchi wa Kisemvule wameanza kunufaika matokeo chanya ya Mradi huo, wakieleza kupungua kwa gharama za matumizi ya nishati na urahisi wa upatikanaji wa gesi asilia kupitia mifumo ya malipo ya simu.

Mradi huo unaendelea kuwa mfano wa utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Nishati Safi ukionesha namna uwekezaji wa kimkakati unavyoweza kubadilisha maisha ya Wanancha ili kulinda mazingira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ngazi ya jamii.

MWIS

Mkaa Mbadala Mkombozi Matumizi ya Nishati kwa Watanzania
Newsletters

Ni kuelekea asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034

Mkaa Mbadala Mkombozi Matumizi ya Nishati kwa Watanzania

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya mkaa mbadala unaozalishwa nchini ili kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034 kulingana na Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya nishati safi hapa nchini.

Wito huo umetolewa leo Februari 28, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu akiwa ameongoza na Menejimenti ya REA wakati walipotembelea kiwanda cha Shirika la Mzinga kujionea kuhusu uzalishaji wa teknolojia ya mkaa mbadala unaofanywa na Shirika hilo mkoani Morogoro.

Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu ameeleza kuwa Serikali kupitia REA imehamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia katika ajenda ya Kitaifa ya nishati safi ya kupikia katika kuwawezesha Watanzania wanatumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.

"Matumizi ya mkaa mbadala yatatuwezesha kuweza kufikia asilimia 80 ya watanzania kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034. Ni lazima tuipe nguvu ajenda hii kwa kuwa inakwenda kuwa mkombozi kwa nchi yetu, " Ameongeza Balozi Kingu.

Kwa upande wake, Brigedia Jenerali Seif Hamisi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mzinga ameishukuru REA kwa fursa hiyo ya kuwatembelea katika kiwanda chao cha Mzinga na kujionea namna uzalishaji wa mkaa mbadala unavyofanywa na kiwanda hicho mkoani humo.

Amesema, ni matarajio yao kuwa kiwanda hicho kinakwenda kukidhi mahitaji ya watumiaji wa mkaa mbadala kwa kuwa kwa sasa wanaendelea kufanya tafiti na kuzungumza na wadau mbalimbali ikiwemo REA ili kuhakikisha wanapata teknolojia za kisasa zitakazowezesha kuanza kuzalisha mkaa huo kwa wingi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa mkaa mbadala katika kiwanda cha Mzinga Mha. Amiri Msangi, ameeleza kuwa kwa sasa kiwanda kinaendekea kufanya tafiti wa teknolojia  teknolojia bora na rafiki ya uzalishaji wa mkaa mbadala ili uzalishaji utakapoanza na kuwa mkubwa uweze kuleta tija kwa Watanzania na kuongeza kipato kwa shirika.

Mwisho.

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma
Events

Ni tuzo ya ubora katika kushughulikia malalamiko kwa Wananchi na kutoa mrejesho

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

RSS
«March 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2324252627281
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
303112345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top