Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA
Frank A. Mugogo 478

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.
 
Mhandisi Hassan ametoa pongezi hizo leo tarehe 27 Machi, 2025 wakati akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Mkutano wa Pili (Kikao cha Sita) cha Baraza hilo, mkoa Morogoro katika ukumbi wa Magadu.
 
Mha. Saidy amesema miaka minne iliyopita; Baraza la Wafanyakazi lilikuwa na idadi ndogo ya Wajumbe na ambao wengi wao walikuwa wakitoka kwenye Menejimenti, tofauti na sasa ambapo Wajumbe wengi wanatoka kwenye kundi la Watumishi wote.
 
“Wageni na Wajumbe wa Baraza hili ni Baraza letu la Pili, Mwezi Desemba, 2021 ndiyo tulianza Baraza letu la kwanza, napenda kuwapongeza kwa ufanisi na kujituma kwenu kwa kuwa ninyi (Watumishi) ndiyo chanzo cha mafanikio ya Taasisi yetu.”Amesema, Mhandisi, Saidy.
 
Mhandisi Saidy ametoa wito kwa Watumishi (Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi) kuwa huru kutoa michango ya mawazo yao kwa yale mambo ambayo yataongeza tija kwenye Taasisi (Wakala) na kwa Watumishi.
 
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilima Watu kutoka Wizara ya Nishati, Bi. Zaina Mlawa amesem Wizara ya Nishati (Makao Makuu) itaendelea kuzisimamia Taasisi zake zote  zilizochini yake (Ikiwemo REA) ili kuendelea kuongeza tija na ufanisi kwa utoaji wa huduma kwa umma.
 
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza Kuu TUGHE Taifa, Dkt. Elias Mtungilwa ametoa pongezi nyingi kwa Baraza la Wafanyakazi la REA kwa kuwa na uwinao mzuri wa Wajumbe kutoka makundi yote Watumishi pamoja na kuzingatia masuala ya jinsia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top