Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA
Frank A. Mugogo 656

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.
 
Mhandisi Hassan ametoa pongezi hizo leo tarehe 27 Machi, 2025 wakati akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Mkutano wa Pili (Kikao cha Sita) cha Baraza hilo, mkoa Morogoro katika ukumbi wa Magadu.
 
Mha. Saidy amesema miaka minne iliyopita; Baraza la Wafanyakazi lilikuwa na idadi ndogo ya Wajumbe na ambao wengi wao walikuwa wakitoka kwenye Menejimenti, tofauti na sasa ambapo Wajumbe wengi wanatoka kwenye kundi la Watumishi wote.
 
“Wageni na Wajumbe wa Baraza hili ni Baraza letu la Pili, Mwezi Desemba, 2021 ndiyo tulianza Baraza letu la kwanza, napenda kuwapongeza kwa ufanisi na kujituma kwenu kwa kuwa ninyi (Watumishi) ndiyo chanzo cha mafanikio ya Taasisi yetu.”Amesema, Mhandisi, Saidy.
 
Mhandisi Saidy ametoa wito kwa Watumishi (Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi) kuwa huru kutoa michango ya mawazo yao kwa yale mambo ambayo yataongeza tija kwenye Taasisi (Wakala) na kwa Watumishi.
 
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilima Watu kutoka Wizara ya Nishati, Bi. Zaina Mlawa amesem Wizara ya Nishati (Makao Makuu) itaendelea kuzisimamia Taasisi zake zote  zilizochini yake (Ikiwemo REA) ili kuendelea kuongeza tija na ufanisi kwa utoaji wa huduma kwa umma.
 
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza Kuu TUGHE Taifa, Dkt. Elias Mtungilwa ametoa pongezi nyingi kwa Baraza la Wafanyakazi la REA kwa kuwa na uwinao mzuri wa Wajumbe kutoka makundi yote Watumishi pamoja na kuzingatia masuala ya jinsia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top