Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA
Frank A. Mugogo 164

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.
 
Mhandisi Hassan ametoa pongezi hizo leo tarehe 27 Machi, 2025 wakati akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Mkutano wa Pili (Kikao cha Sita) cha Baraza hilo, mkoa Morogoro katika ukumbi wa Magadu.
 
Mha. Saidy amesema miaka minne iliyopita; Baraza la Wafanyakazi lilikuwa na idadi ndogo ya Wajumbe na ambao wengi wao walikuwa wakitoka kwenye Menejimenti, tofauti na sasa ambapo Wajumbe wengi wanatoka kwenye kundi la Watumishi wote.
 
“Wageni na Wajumbe wa Baraza hili ni Baraza letu la Pili, Mwezi Desemba, 2021 ndiyo tulianza Baraza letu la kwanza, napenda kuwapongeza kwa ufanisi na kujituma kwenu kwa kuwa ninyi (Watumishi) ndiyo chanzo cha mafanikio ya Taasisi yetu.”Amesema, Mhandisi, Saidy.
 
Mhandisi Saidy ametoa wito kwa Watumishi (Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi) kuwa huru kutoa michango ya mawazo yao kwa yale mambo ambayo yataongeza tija kwenye Taasisi (Wakala) na kwa Watumishi.
 
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilima Watu kutoka Wizara ya Nishati, Bi. Zaina Mlawa amesem Wizara ya Nishati (Makao Makuu) itaendelea kuzisimamia Taasisi zake zote  zilizochini yake (Ikiwemo REA) ili kuendelea kuongeza tija na ufanisi kwa utoaji wa huduma kwa umma.
 
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza Kuu TUGHE Taifa, Dkt. Elias Mtungilwa ametoa pongezi nyingi kwa Baraza la Wafanyakazi la REA kwa kuwa na uwinao mzuri wa Wajumbe kutoka makundi yote Watumishi pamoja na kuzingatia masuala ya jinsia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top