Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016
Aodax K. Nshala 6791

REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016

Yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Lindi Katika Viwanja vya Ngongo

Event date: 8/1/2016 - 8/8/2016 Export event

Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nane Nane) yalifanyika Mkoani Lindi katika Viwanja vya Ngongo kuanzia tarehe 01/08/2016 hadi 08/08/2016. Ujumbe wa maonesho hayo ulikuwa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni Nguzo ya Maendeleo, Kijana Shiriki Kikamilifu “Hapa Kazi tu”.

Katika maonesho hayo Wakala ulishiriki pamoja na wadau ambao ni:

  • EFFORT - Walioonesha teknolojia ya kutengeneza mkaa mbadala;
  • Moody Solar - Walioonesha teknolojia ya Umeme Jua;
  • Davis & Shertilif - Walioonesha teknolojia za Vifaa vya umeme jua (zikilenga pampu ya kumwagilia maji);
  • Oryx Gas Ltd - Walioonesha teknolojia ya Gesi ya kupikia majumbani; na
  • Ok Electrical and Electronics Services LTD - Walioonesha teknolojia ya vifaa vya usambazaji wa umeme vijijini.

Katika maonesho hayo, Wakala ulipata fursa ya kuelezea mpango wake wa kusambaza umeme vijijini na kuonesha picha za wanufaika wa miradi ya REA katika mikoa ya Lindi na Mtwara pamoja na mikoa mingine (video documentary) na kusikiliza kero na maoni ya wananchi kuhusu miradi ya kusambaza nishati bora vijijini.

Wananchi wengi waliofika katika banda la Wakala walitoa pongezi na shukrani kwa kupelekewa huduma ya umeme kupitia miradi ya kusambaza umeme vijijini. Hata hivyo, walijitokeza baadhi ya wananchi waliolalamikia baadhi ya vijiji vyao kutofikiwa na miundo mbinu ya umeme na kuomba maelezo ya mpango endelevu wa kusambaza umeme vijiji vyote Tanzania Bara.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top