Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016
Aodax K. Nshala 6812

REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016

Yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Lindi Katika Viwanja vya Ngongo

Event date: 8/1/2016 - 8/8/2016 Export event

Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nane Nane) yalifanyika Mkoani Lindi katika Viwanja vya Ngongo kuanzia tarehe 01/08/2016 hadi 08/08/2016. Ujumbe wa maonesho hayo ulikuwa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni Nguzo ya Maendeleo, Kijana Shiriki Kikamilifu “Hapa Kazi tu”.

Katika maonesho hayo Wakala ulishiriki pamoja na wadau ambao ni:

  • EFFORT - Walioonesha teknolojia ya kutengeneza mkaa mbadala;
  • Moody Solar - Walioonesha teknolojia ya Umeme Jua;
  • Davis & Shertilif - Walioonesha teknolojia za Vifaa vya umeme jua (zikilenga pampu ya kumwagilia maji);
  • Oryx Gas Ltd - Walioonesha teknolojia ya Gesi ya kupikia majumbani; na
  • Ok Electrical and Electronics Services LTD - Walioonesha teknolojia ya vifaa vya usambazaji wa umeme vijijini.

Katika maonesho hayo, Wakala ulipata fursa ya kuelezea mpango wake wa kusambaza umeme vijijini na kuonesha picha za wanufaika wa miradi ya REA katika mikoa ya Lindi na Mtwara pamoja na mikoa mingine (video documentary) na kusikiliza kero na maoni ya wananchi kuhusu miradi ya kusambaza nishati bora vijijini.

Wananchi wengi waliofika katika banda la Wakala walitoa pongezi na shukrani kwa kupelekewa huduma ya umeme kupitia miradi ya kusambaza umeme vijijini. Hata hivyo, walijitokeza baadhi ya wananchi waliolalamikia baadhi ya vijiji vyao kutofikiwa na miundo mbinu ya umeme na kuomba maelezo ya mpango endelevu wa kusambaza umeme vijiji vyote Tanzania Bara.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top