Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016
Aodax K. Nshala 6795

REA Katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima - Nane Nane 2016

Yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Lindi Katika Viwanja vya Ngongo

Event date: 8/1/2016 - 8/8/2016 Export event

Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nane Nane) yalifanyika Mkoani Lindi katika Viwanja vya Ngongo kuanzia tarehe 01/08/2016 hadi 08/08/2016. Ujumbe wa maonesho hayo ulikuwa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni Nguzo ya Maendeleo, Kijana Shiriki Kikamilifu “Hapa Kazi tu”.

Katika maonesho hayo Wakala ulishiriki pamoja na wadau ambao ni:

  • EFFORT - Walioonesha teknolojia ya kutengeneza mkaa mbadala;
  • Moody Solar - Walioonesha teknolojia ya Umeme Jua;
  • Davis & Shertilif - Walioonesha teknolojia za Vifaa vya umeme jua (zikilenga pampu ya kumwagilia maji);
  • Oryx Gas Ltd - Walioonesha teknolojia ya Gesi ya kupikia majumbani; na
  • Ok Electrical and Electronics Services LTD - Walioonesha teknolojia ya vifaa vya usambazaji wa umeme vijijini.

Katika maonesho hayo, Wakala ulipata fursa ya kuelezea mpango wake wa kusambaza umeme vijijini na kuonesha picha za wanufaika wa miradi ya REA katika mikoa ya Lindi na Mtwara pamoja na mikoa mingine (video documentary) na kusikiliza kero na maoni ya wananchi kuhusu miradi ya kusambaza nishati bora vijijini.

Wananchi wengi waliofika katika banda la Wakala walitoa pongezi na shukrani kwa kupelekewa huduma ya umeme kupitia miradi ya kusambaza umeme vijijini. Hata hivyo, walijitokeza baadhi ya wananchi waliolalamikia baadhi ya vijiji vyao kutofikiwa na miundo mbinu ya umeme na kuomba maelezo ya mpango endelevu wa kusambaza umeme vijiji vyote Tanzania Bara.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top