Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 19,530 Mkoani Mara
Frank A. Mugogo 6

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 19,530 Mkoani Mara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530 yenye thamani ya Shilingi milioni 390 katika wilaya sita za mkoa wa Mara ambapo mradi huo utawanufasiha wakazi wa maeneo ya vijijini.

Akizundua mradi huo leo, tarehe 21 Oktoba, 2025 kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali, Evans Mtambi, Mkuu wa wilaya ya Musoma, Mhe. Juma Chikoka amesema Serikali imeweka ruzuku kupunguza gharama ili Wananchi wajaribu matumizi ya nishati hiyo na kuona faida yake ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Mhe. Chikoka amesema Mradi huo wa REA ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini huku Wananchi mkoani humo wakiiomba seijali kusogeza vituo vya kujaza gesi karibu na makazi yao.

Mitungi hiyo yenye ujazo wa kilo 6 kila moja itauzwa kwa bei ya ruzuku ili kuwezesha Wananchi wa maeneo hayo ya vijijini kuanza matumizi ya nishati hiyo na kuachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo yameelezwa kuwa na athari nyingi ikiwemo za kiafya na kimazingira.

Chikoka amesema mitungi hiyo inatarajiwa kusambazwa katika wilaya zote sita (6) za mkoa wa Mara na kueleza kuwa Serikali inatambua athari zinazowakumba Wananchi hasa Wanawake kutokana na matumizi ya kuni na mkaa.

"Serikali inatambua changamoto zinazotokana na matumizi ya kuni na mkaa ukiachana na hili la mabadiliko ya tabia nchi lakini pia kuna suala la afya hivyo ikaona ipo haja ya kuja na mradi huu kwa maslahi mapana ya watu wake," amesema 

Chikoka amewataka wakazi wa mkoa huo kutumia fursa hiyo ili kuweza kujipatia mitungi hiyo na kuanza safari ya matumizi ya nishati ya gesi katika mapishi yao ya kila siku.

Rais Samia Suluhu Hassan tayari alitangaza mkakati wa Serikali wa kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini hadi kufika asilimia 80 mwaka 2034.

Chikoka amesema jamii inapaswa kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na kuhamia kwenye nishati safi ya kupikia kwa maelezo kuwa mbali na faida za kiafya na mazingira pia matumizi ya nishati safi ni gharama nafuu ikilinganishwa na kuni na mkaa.

Akitoa taarifa ya mradi huo katika kijiji cha Etaro wilayani Musoma leo Oktoba 21,2025, Mhandisi wa Miradi kutoka REA, Geofrey Gedo amesema kuwa kwa mujibu wa utafiti waathirika wengi wa matumizi ya nishati isiyokuwa salama ni Wanawake na Watoto jambo ambalo Serikali imeona ipo haja ya kulitafutia ufumbuzi wa kudumu.

"Utafiti uliofanywa mwaka 2016 ulibainisha kuwa watu 33,024 hufarki nchini kila mwaka kabla ya wakati hii ni sawa na asilimia 8.49 ya vifo vyote nchini na vifo hivi hutokana na magonjwa ambayo yanachangiwa na uchafuzi wa hewa ndani ya nyumba huku waathirika wengi wakiwa ni Wanawake na Watoto," amesema.

Amesema takwimu zinaonyesha kuwa matumizi ya kuni kama chanzo kikuu ca nishati ya kupikia nchini bado ni makubwa sana ambapo asilimia 63.5 ya kaya nchini zinatumia kuni kama chanzo cha nishati.

Amefafanua takwimu hizo pia zinaonyesha kuwa matumizi ya mkaa ni asilimia 26.2 huku matumizi ya gesi iliyojazwa kwenye nitungi (LGP) ikiwa ni asilimia 5.1 pekee na umeme ukiwa unatumiwa kwa asilimia 3 huku vyanzo vingine vikiwa ni asilimia 2.2

Amesema kupitia mradi huo wa uuzwaji wa mitungi hiyo kwa bei ya ruzuku utasaidia kupandisha kiwango cha Watu wanaotumia nishati ya gesi nchini hivyo kuondokana na athari zinazotokana na matumizi ya nishati chafu ya kupikia.

"Mitungi hii itauzwa kwa bei ya ruzuku ambayo ni asilimia 50 ambapo kila mtungi pamoja na vifaa vyake utauzwa kwa Sh20,000 hii bei ni rafiki na tunaamini hata zile familia zenye kipato cha chini kitamudu," amesema 

Wakizungumza kwenye uzinduzi huo baadhi ya wakazi wa kijiji cha Etaro wameiomba Serikali kuhakikisha nishati hiyo ya gesi inapatikana kwa ukaribu ili kuepuka gharama za ziada.

"Hapa kwetu angalau kuna sehemu gesi ikiisha unaweza kwenda kujaza kwasababu hapa senta kuna Wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara hii lakini kuna maeneo mengi hakuna gesi hivyo ukihitaji inakubidi usafiri umbali mrefu," amesema Nyangeta Chimwejo.


Eva Willim amesema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi wananchi hasa wa vijijini hawana budi kuanza kutumia nishati ya gesi katika mapishi yao kwa maelezo kuwa upatikanaji wa miti na mkaa hivi sasa umekuwa wa shida.

"Zamani kuni zilikuwa zinapatikana kwa ukaribu zaidi lakini sasa hivi misitu yote imeteketezwa na matumizi ya binadamu, tunashukuru Serikali kutuletea mitungi hii kwani itakuwa ni hamasa kwa wengi kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na kuhamia kwenye gesi," amesema 

Alex Kagere amesema usambazaji huo wa mitungi ya gesi maeneo ya vijijini ni mkombozi kwa wakazi wa vijijini hasa wanawake ambao wamekuwa wakitumia kuni wakati wa mapishi.

"Huu mradi ni mzuri kwasababu nyingi kwanza mabadiliko ya tabia nchi yamesababisha nishati ya kuni kukosekana lakini madhara yanayotokana na mtumizi ya kuni pia ni mengi hivyo nitoe tu msisitizo Serikali iangalie namna ili gesi iwe inapatikana kwa ukaribu huku vijijini ili tukitaka kujaza tusipate shida," amesema 

Amesema uharibifu wa mazingira pamoja na mambo mengine unasababishwa na matumizi ya nishati isiyo salama na ndio maana Rais Samia  amekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwani ni  faida kubwa kwa afya ya jamii na mazingira kwa ujumla.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top