Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wakandarasi Kamilisheni Miradi Kwa Wakati – Mkurugenzi Mkuu REA
Frank A. Mugogo 723

Wakandarasi Kamilisheni Miradi Kwa Wakati – Mkurugenzi Mkuu REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewaagiza wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini kukamilisha kazi kwa muda waliopewa kwa mujibu wa mikataba.

Agizo hilo amelitoa leo tarehe 04 Januari, 2024 wilayani Korogwe akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili mkoa wa Tanga.

"Wanaochelewesha miradi wanawazuia wananchi kupata huduma kwa wakati kwa sababu hiyo hakuna nyongeza ya muda itakayotolewa kwa wakandarasi ambao watachelewa kukamilisha Miradi", alisema.

Aidha, Mhandisi Saidy aliwataka Wananchi kulinda miundombinu ya umeme na wakati huo huo ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati ya umeme  kuboresha vipato vyao.

Mkurugenzi Mkuu wa REA yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kukagua maendeleo ya mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika vijiji vya wilaya ya Korogwe mkoani humo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
15161718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top