Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wakandarasi Kamilisheni Miradi Kwa Wakati – Mkurugenzi Mkuu REA
Frank A. Mugogo 393

Wakandarasi Kamilisheni Miradi Kwa Wakati – Mkurugenzi Mkuu REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewaagiza wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini kukamilisha kazi kwa muda waliopewa kwa mujibu wa mikataba.

Agizo hilo amelitoa leo tarehe 04 Januari, 2024 wilayani Korogwe akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili mkoa wa Tanga.

"Wanaochelewesha miradi wanawazuia wananchi kupata huduma kwa wakati kwa sababu hiyo hakuna nyongeza ya muda itakayotolewa kwa wakandarasi ambao watachelewa kukamilisha Miradi", alisema.

Aidha, Mhandisi Saidy aliwataka Wananchi kulinda miundombinu ya umeme na wakati huo huo ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati ya umeme  kuboresha vipato vyao.

Mkurugenzi Mkuu wa REA yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kukagua maendeleo ya mradi wa usambazaji nishati ya umeme katika vijiji vya wilaya ya Korogwe mkoani humo.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top