Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Kuanza Kupeleka Umeme Kwenye Vitongoji Mwaka 2024
Frank A. Mugogo 1668

REA Kuanza Kupeleka Umeme Kwenye Vitongoji Mwaka 2024

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umekusudia kuanzia mwaka 2024 kufikisha miundombinu ya umeme hadi kwenye vitongoji baada ya kukamilisha utekelezwaji wa mradi wa kuunganisha huduma hiyo kwenye vijiji vyote nchini.

Imeelezwa kuwa, hadi sasa usambazaji wa umeme vijijini umefikia asilimia 80 tangu kuanza kwa utekelezaji wa Mradi wa Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili  mwezi Julai 2018 wa kufikisha umeme vijijini. Ni Vijiji 758 tu vilivyobaki kati ya Vijiji 12,315 vilivyopo nchi nzima; na wakandarasi wote waliopewa zabuni wamefikia asilimia 75. Ifikapo mwisho wa mwezi Februari 2024 wakandarasi wote watakuwa wamekamilisha utekelezaji wa miradi yao.

Akizungumza hivi karibu mkoani Pwani baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo na kufanya tathimini ya mwaka mzima wa utekelezaji mradi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi Thomas Mmbaga alisema kuanzia mwaka huu 2024, Wakala utakuwa unapeleka umeme katika ngazi ya vitongoji.

“Mkakati unakuja, baada ya miundombinu kufikishwa katika kila makao makuu ya kijiji, vijiji vingi ni vikubwa na vina vitongoji kuanzia vitano na kuendelea; mkakati wa kufikisha umeme katika vitongoji vyote utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha”, alisema.

Alisema baada ya kukamilisha vijiji 758 vilivyofikiwa na huduma ya umeme, watapeleka miundombinu hiyo katika jumla ya vitongoji 3,060.

Awali, Katika ukaguzi huo Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati ya Umeme Vijijini (REB); Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu alisema ameridhishwa na namna taasisi hiyo inavyosimamia utekelezwaji wa mradi huo. 

“Nimeona mafanikio makubwa katika Wilaya tatu za mkoa wa Pwani nilizotembelea nikianza na Mkuranga, Kisarawe, Kibiti na Rufiji. Huduma imefika zaidi ya asilimia 90; bado vijiji vichache havijafikiwa kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kuzungukwa na maeneo oevu yenye majimaji”, alisema Balozi Kingu.

Alisema kwa vijiji vilivyofikiwa na huduma hiyo, ni muhimu kwa Wananchi kuanza kuchangamkia kutumia fursa ili iwe kichocheo na chachu katika kukuza shughuli zao za kiuchumi.

"Kama Mwenyekiti wa Bodi nitahakikisha natoa uongozi kwa REA kuona ndoto zetu zinafikiwa za kufikisha huduma ya umeme vijiji vyote nchini katika kutimiza azma ya serikali", alisema. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini alisema bado ataendelea kufanya ziara za mara kwa mara kukagua maendeleo ya utekelezwaji wa miradi katika mikoa mbalimbali lengo likiwa kuhakikisha shughuli hiyo inakamilika ifikapo Juni 2024.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top