Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy, wamemtembelea Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina na kujadiliana kuhusu utekelezwaji miradi ya umeme vijijini, wilayani humo.
Waziri wa Nishati January Makamba amewaelekeza viongozi na wafanyakazi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza nguvu katika aina nyingine za nishati kama inavyofanyika kwenye umeme.
REA News Magazine Issue #3, November 2021 / Jarida la Wakala wa Nishati Vijijini, REA News Toleo #3, Novemba 2021.
Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Medard Kalemani amesema kipaumbele cha Serikali katika kusambaza nishati vijijini ni kupeleka umeme katika vitongoji.
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imefanya ziara ya siku moja katika Mradi wa Umeme wa Julius Nyerere uliopo Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani kwa ajili ya kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao ukikamilika utawezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini.
Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Merdad Kalemani amezindua Mradi wa Ujazilizi Fungu la Pili tarehe 24 Septemba 2020. Mradi huu unalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme kwenye vitongoji katika vijiji vilivyofikiwa na miundombinu ya umeme.
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) haijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida unayotekelezwa na Kampuni ya Emerc and Dynamic Engineering.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amekipongeza kikosi cha Suma JKT ambacho kimepewa kazi kujenga miundombinu ya kusambaza umeme katika kata ya Kwa Mtoro na Farkwa.