Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini Sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji
Admin.Frank Mugogo 5388

Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini Sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Merdad Kalemani amezindua Mradi wa Ujazilizi Fungu la Pili tarehe 24 Septemba 2020. Mradi huu unalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme kwenye vitongoji katika vijiji vilivyofikiwa na miundombinu ya umeme.

Akizindua Mradi huo katika Kitongoji cha Ufuluma Senta, Wilaya ya Uyui na Kitongoji cha Migombani, Wilaya ya Nzega, Dkt. Kalemani alisema vitongoji ambavyo havina umeme vitaanza kusambaziwa umeme sasa. “Mpango halisi wa kuanza kupeleka umeme kwenye vitongoji unaanza rasmi leo hapa Mkoani Tabora” alisema.

Alisema jumla ya vitongoji 1,103 na wateja wa awali 69,079 wataunganishiwa huduma ya umeme kwa kipindi cha miezi 9 ya utekelezaji wa Mradi huo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dr. Philemon Sengati alitoa wito kwa wananchi kutumia vizuri fursa ya upatikanaji wa huduma ya umeme ili kufanikisha malengo ya Serikali kufikia uchumi wa viwanda.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo aliwahimiza wananchi kutumia nishati ya umeme kwa ajili ya kuongeza kipato kwa kuanzisha shughuli za uzalishaji mali ili kubadili mfumo duni wa maisha ya vijijini.

Mradi huu unafadhiliwa na Serikli za Tanzania, Norway na Sweden pamoja na Umoja wa Ulaya kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini (REF) na utagharimu Shilingi Bilioni 142. Utatekelezwa katika mikoa tisa (9) ya Dodoma, Kilimanjaro, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Singida, Pwani, Tanga na Mbeya.

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top