Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini Sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji
Admin.Frank Mugogo 5456

Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini Sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Merdad Kalemani amezindua Mradi wa Ujazilizi Fungu la Pili tarehe 24 Septemba 2020. Mradi huu unalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme kwenye vitongoji katika vijiji vilivyofikiwa na miundombinu ya umeme.

Akizindua Mradi huo katika Kitongoji cha Ufuluma Senta, Wilaya ya Uyui na Kitongoji cha Migombani, Wilaya ya Nzega, Dkt. Kalemani alisema vitongoji ambavyo havina umeme vitaanza kusambaziwa umeme sasa. “Mpango halisi wa kuanza kupeleka umeme kwenye vitongoji unaanza rasmi leo hapa Mkoani Tabora” alisema.

Alisema jumla ya vitongoji 1,103 na wateja wa awali 69,079 wataunganishiwa huduma ya umeme kwa kipindi cha miezi 9 ya utekelezaji wa Mradi huo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dr. Philemon Sengati alitoa wito kwa wananchi kutumia vizuri fursa ya upatikanaji wa huduma ya umeme ili kufanikisha malengo ya Serikali kufikia uchumi wa viwanda.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo aliwahimiza wananchi kutumia nishati ya umeme kwa ajili ya kuongeza kipato kwa kuanzisha shughuli za uzalishaji mali ili kubadili mfumo duni wa maisha ya vijijini.

Mradi huu unafadhiliwa na Serikli za Tanzania, Norway na Sweden pamoja na Umoja wa Ulaya kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini (REF) na utagharimu Shilingi Bilioni 142. Utatekelezwa katika mikoa tisa (9) ya Dodoma, Kilimanjaro, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Singida, Pwani, Tanga na Mbeya.

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top