Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
LINDI NA MTWARA WAPATA MIJI WASHIRIKA KUTOKA NORWAY
Host 13384

LINDI NA MTWARA WAPATA MIJI WASHIRIKA KUTOKA NORWAY

Waziri wa Nishati na madini, Profesa Sospeter Muhongo na viongozi wa miji miwili ya Hammerfest na Sandnessjoen iliyoko nchini Norway wamekubaliana kuanzisha ushirikiano baina ya miji hiyo na ile ya Lindi na Mtwara.

Uamuzi huo umefikiwa katika mkutano baina ya viongozi wa miji hiyo na ujumbe wa wizara ya nishati na madini nchini Norway ambapo wamekubaliana kukutana mwezi ujao kuweka mikakati ya ushirikiano huo.

Katika makubaliano hayo viongozi kutoka pande zote wamekubaliana kuwa mji wa Harmmerfest utashirikiana na Lindi na ule wa Sandnessjoen utashirikiana na Mtwara, ushirikiano ambao unalenga kuzitumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi.

Akizungumza mara baada ya kufikia makubaliano hayo Waziri wa Nishati na Madini Profesa Muhongo amesema ili kuhakikisha mikoa ya kusini inanufaika na rasilimali zake, Serikali imeamua kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kutimiza azma hiyo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa wavuvi katika mji wa Sandnessjoen amesema uhusiano mzuri kati ya serikali na makampuni ya mafuta umechangia kubadilisha historia ya watu wa maeneo hayo ikiwemo kuwawezesha kukua kichumi na kuwasaidia kupata huduma mbalimbali za kijamii.

Akizungumzia umuhimu wa makampuni ya mafuta katita mji wa Sandnessjoen Meya wa mji huo Bard Anders Lango amesema, kwa kiasi kikubwa mapato ya mji huo yanatokana na mafuta.

Aidha Lango ameongeza kuwa asilimia ishirini na mbili ya mapato yanayotokana na Mafuta inatumika kutoa huduma muhimu za kijamii katika sekta za afya na elimu.

Naye Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Mafuta la BP Olav Fjellsa amesema moja ya mbinu ambazo zimeliwezesha shirika hilo kujenga mahusiano mema na jamii ni kuhakikisha yanatoa misaada katika maeneo husika, kuwekeana mikataba mizuri pamoja na kujihusisha na ununuzi wa bidhaa za wazawa.

Kuanzishwa kwa ushirikiano baina ya miji hiyo na mikoa ya kusini kutasaidia kufungua ukurasa mpya wa mahusiano na hiyvo kuwezesha wananchi kuwa sehemu ya mafanikio ya kuanzishwa kwa miradi ya umma katika maeneo yao.

Kabla ya ugunduzi wa Gesi na Mafuta miji hiyo miwili ilikuwa ikijishughulisha na uvuvi, kabla ya Serikali ya Norway kuamua kuanzisha shughuli za uchimbaji wa gesi na mafuta baada ya kufikia makubaliano na wananchi wa maeneo hayo.


Imeandaliwa na:

Nuru I. Mwasampeta
Afisa Habari
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
20212223242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top