Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI
Aodax K. Nshala 11184

MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI

Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi na Washirika wa Maendeleo nchini, wameshauriwa kutumia fursa zilizopo katika sekta ya nishati hususani umeme kushirikiana na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ili kuongeza kasi ya kuviunganisha vijiji vingi zaidi na umeme, ikiwemo kuwezesha mapinduzi ya maendeleo kupitia nishati hiyo.

Hayo yamebainishwa kwa nyakati tofauti kwenye kikao kazi kilichoandaliwa na REA, kikijumuisha Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi, Washirika wa Maendeleo, Washirika katika tasnia ya nishati, na wawakilishi kutoka Wizara na Taasisi za Serikali, kwa lengo la kujadili na kuangalia namna sekta hizo zinavyoweza kushirikiana pamoja ili kuongeza nguvu ya kuhakikisha Tanzania hususan vijiji vinaunganishwa na nishati ya umeme ili kuchochea shughuli za kiuchumi vijijini.

Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava, alisema, miradi ya kuviunganisha vijiji na nishati ya umeme ni eneo linalohitaji kuendelezwa kwa ushirikiano na wadau hao ili kuongeza kasi ya uunganishaji umeme.

Alisema kuwa, tangu Wakala huo kuanzishwa mwaka 2007 kasi ya kuviunganisha vijiji na umeme imeongezeka, na kuongeza kuwa, jitihada kubwa imekwishafanywa na Serikali na endapo wadau hao wataunganisha nguvu, azma ya serikali kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030 taifa zima liwe limeunganishwa na nishati hiyo litafikiwa haraka kwa kuwa REA itakuwa na vyanzo vingi vya fedha.

Mwihava aliongeza kuwa, serikali imefanikiwa kuimarisha miundombinu ya uzalishaji umeme jambo ambalo limewezesha kiwango cha uzalishaji kuongezaka kutoka megawati 891 mwaka 2005 hadi 1,226.3, Machi 2015.

“Ikiwa vijiji vyetu vitaunganishwa na nishati hiyo, hali hiyo itachochea shughuli za kiuchumi kufanyika ikiwemo kuanzishwa kwa viwanda vidogo katika maeneo ya vijijini, na kuongeza huduma za kisasa za kiuchumi zinazotumia nishati hiyo. Umeme ni maendeleo na ili tuendelee tunahitaji umeme,” alisema Mwihava.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Edmund Mkwawa, alieleza kuwa, endapo wadau hao watashirikiana na REA, mradi huo utaleta matokeo makubwa zaidi ya yaliyopatikana sasa na hivyo kuweza kuyafikia maeneo ambayo hayajafikiwa na nishati hiyo. Aliongeza kuwa, zipo fursa nyingi ambazo taasisi hizo zinaweza kuzitumia kupitia miradi mbalimbali ambayo itawezesha kupata faida na hivyo, kikao hicho kitawawezesha wadau hao kutambua fursa hizo.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa REA, Dkt. Lutengano Mwakahesya alitumia fursa hiyo kuwashukuru wadau wote ambao wamewezesha Wakala huo kuunganisha miji, vijiji na nishati hiyo kufikia asilimia 40 na kueleza kuwa, Wakala huo utaendelea kutafuta wafadhili ili kuweza kufanikisha malengo yake ya kuhakikisha kwamba taifa linaunganishwa na umeme.

Aliongeza kuwa, serikali peke yake haiwezi kufanya kazi hiyo na kueleza kuwa, uhakika wa uwepo wa umeme utawezesha wananchi wengi zaidi kujiingiza katika shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi anayeshughulikia nishati kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Stella Mandago, alizitaka taasisi hizo kufanya kazi na Wakala huo kwani zipo fursa nyingi na hivyo itawezesha taasisi hizo kupanua wigo wa shughuli zao kiuchumi kupitia nishati ya umeme.

Na Asteria Muhozya
MEM News Bullettin Toleo No. 78

Share

Print

Documents to download

«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top