Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI
Aodax K. Nshala 11100

MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI

Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi na Washirika wa Maendeleo nchini, wameshauriwa kutumia fursa zilizopo katika sekta ya nishati hususani umeme kushirikiana na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ili kuongeza kasi ya kuviunganisha vijiji vingi zaidi na umeme, ikiwemo kuwezesha mapinduzi ya maendeleo kupitia nishati hiyo.

Hayo yamebainishwa kwa nyakati tofauti kwenye kikao kazi kilichoandaliwa na REA, kikijumuisha Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi, Washirika wa Maendeleo, Washirika katika tasnia ya nishati, na wawakilishi kutoka Wizara na Taasisi za Serikali, kwa lengo la kujadili na kuangalia namna sekta hizo zinavyoweza kushirikiana pamoja ili kuongeza nguvu ya kuhakikisha Tanzania hususan vijiji vinaunganishwa na nishati ya umeme ili kuchochea shughuli za kiuchumi vijijini.

Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava, alisema, miradi ya kuviunganisha vijiji na nishati ya umeme ni eneo linalohitaji kuendelezwa kwa ushirikiano na wadau hao ili kuongeza kasi ya uunganishaji umeme.

Alisema kuwa, tangu Wakala huo kuanzishwa mwaka 2007 kasi ya kuviunganisha vijiji na umeme imeongezeka, na kuongeza kuwa, jitihada kubwa imekwishafanywa na Serikali na endapo wadau hao wataunganisha nguvu, azma ya serikali kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030 taifa zima liwe limeunganishwa na nishati hiyo litafikiwa haraka kwa kuwa REA itakuwa na vyanzo vingi vya fedha.

Mwihava aliongeza kuwa, serikali imefanikiwa kuimarisha miundombinu ya uzalishaji umeme jambo ambalo limewezesha kiwango cha uzalishaji kuongezaka kutoka megawati 891 mwaka 2005 hadi 1,226.3, Machi 2015.

“Ikiwa vijiji vyetu vitaunganishwa na nishati hiyo, hali hiyo itachochea shughuli za kiuchumi kufanyika ikiwemo kuanzishwa kwa viwanda vidogo katika maeneo ya vijijini, na kuongeza huduma za kisasa za kiuchumi zinazotumia nishati hiyo. Umeme ni maendeleo na ili tuendelee tunahitaji umeme,” alisema Mwihava.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Edmund Mkwawa, alieleza kuwa, endapo wadau hao watashirikiana na REA, mradi huo utaleta matokeo makubwa zaidi ya yaliyopatikana sasa na hivyo kuweza kuyafikia maeneo ambayo hayajafikiwa na nishati hiyo. Aliongeza kuwa, zipo fursa nyingi ambazo taasisi hizo zinaweza kuzitumia kupitia miradi mbalimbali ambayo itawezesha kupata faida na hivyo, kikao hicho kitawawezesha wadau hao kutambua fursa hizo.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa REA, Dkt. Lutengano Mwakahesya alitumia fursa hiyo kuwashukuru wadau wote ambao wamewezesha Wakala huo kuunganisha miji, vijiji na nishati hiyo kufikia asilimia 40 na kueleza kuwa, Wakala huo utaendelea kutafuta wafadhili ili kuweza kufanikisha malengo yake ya kuhakikisha kwamba taifa linaunganishwa na umeme.

Aliongeza kuwa, serikali peke yake haiwezi kufanya kazi hiyo na kueleza kuwa, uhakika wa uwepo wa umeme utawezesha wananchi wengi zaidi kujiingiza katika shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi anayeshughulikia nishati kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Stella Mandago, alizitaka taasisi hizo kufanya kazi na Wakala huo kwani zipo fursa nyingi na hivyo itawezesha taasisi hizo kupanua wigo wa shughuli zao kiuchumi kupitia nishati ya umeme.

Na Asteria Muhozya
MEM News Bullettin Toleo No. 78

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print

Documents to download

«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top