Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI
Aodax K. Nshala 11178

MEM NEWS BULLETTIN: REA YATAKA USHIRIKIANO TAASISI ZA KIFEDHA, SEKTA BINAFSI

Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi na Washirika wa Maendeleo nchini, wameshauriwa kutumia fursa zilizopo katika sekta ya nishati hususani umeme kushirikiana na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ili kuongeza kasi ya kuviunganisha vijiji vingi zaidi na umeme, ikiwemo kuwezesha mapinduzi ya maendeleo kupitia nishati hiyo.

Hayo yamebainishwa kwa nyakati tofauti kwenye kikao kazi kilichoandaliwa na REA, kikijumuisha Taasisi za Kifedha, Sekta Binafsi, Washirika wa Maendeleo, Washirika katika tasnia ya nishati, na wawakilishi kutoka Wizara na Taasisi za Serikali, kwa lengo la kujadili na kuangalia namna sekta hizo zinavyoweza kushirikiana pamoja ili kuongeza nguvu ya kuhakikisha Tanzania hususan vijiji vinaunganishwa na nishati ya umeme ili kuchochea shughuli za kiuchumi vijijini.

Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava, alisema, miradi ya kuviunganisha vijiji na nishati ya umeme ni eneo linalohitaji kuendelezwa kwa ushirikiano na wadau hao ili kuongeza kasi ya uunganishaji umeme.

Alisema kuwa, tangu Wakala huo kuanzishwa mwaka 2007 kasi ya kuviunganisha vijiji na umeme imeongezeka, na kuongeza kuwa, jitihada kubwa imekwishafanywa na Serikali na endapo wadau hao wataunganisha nguvu, azma ya serikali kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030 taifa zima liwe limeunganishwa na nishati hiyo litafikiwa haraka kwa kuwa REA itakuwa na vyanzo vingi vya fedha.

Mwihava aliongeza kuwa, serikali imefanikiwa kuimarisha miundombinu ya uzalishaji umeme jambo ambalo limewezesha kiwango cha uzalishaji kuongezaka kutoka megawati 891 mwaka 2005 hadi 1,226.3, Machi 2015.

“Ikiwa vijiji vyetu vitaunganishwa na nishati hiyo, hali hiyo itachochea shughuli za kiuchumi kufanyika ikiwemo kuanzishwa kwa viwanda vidogo katika maeneo ya vijijini, na kuongeza huduma za kisasa za kiuchumi zinazotumia nishati hiyo. Umeme ni maendeleo na ili tuendelee tunahitaji umeme,” alisema Mwihava.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Edmund Mkwawa, alieleza kuwa, endapo wadau hao watashirikiana na REA, mradi huo utaleta matokeo makubwa zaidi ya yaliyopatikana sasa na hivyo kuweza kuyafikia maeneo ambayo hayajafikiwa na nishati hiyo. Aliongeza kuwa, zipo fursa nyingi ambazo taasisi hizo zinaweza kuzitumia kupitia miradi mbalimbali ambayo itawezesha kupata faida na hivyo, kikao hicho kitawawezesha wadau hao kutambua fursa hizo.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa REA, Dkt. Lutengano Mwakahesya alitumia fursa hiyo kuwashukuru wadau wote ambao wamewezesha Wakala huo kuunganisha miji, vijiji na nishati hiyo kufikia asilimia 40 na kueleza kuwa, Wakala huo utaendelea kutafuta wafadhili ili kuweza kufanikisha malengo yake ya kuhakikisha kwamba taifa linaunganishwa na umeme.

Aliongeza kuwa, serikali peke yake haiwezi kufanya kazi hiyo na kueleza kuwa, uhakika wa uwepo wa umeme utawezesha wananchi wengi zaidi kujiingiza katika shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi anayeshughulikia nishati kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Stella Mandago, alizitaka taasisi hizo kufanya kazi na Wakala huo kwani zipo fursa nyingi na hivyo itawezesha taasisi hizo kupanua wigo wa shughuli zao kiuchumi kupitia nishati ya umeme.

Na Asteria Muhozya
MEM News Bullettin Toleo No. 78

Share

Print

Documents to download

«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top