Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga
Aodax K. Nshala 101

Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Kati ya Zaidi ya Vijivi 12,000 Nchi Nzima

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema Vijiji 151 tu nchi nzima ndio ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 ambapo wilayani Ludewa mkoani Njombe vimebaki Vijiji nane.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo jana tarehe 19 Julai 2024 wakati wa ziara ya kikazi katika Vijiji vya Lubonde na Maweni wilayani Ludewa mkoani Njombe akikagua miradi ya nishati.

Wakati wa ziara hiyo Mhe. Kapinga alifanikisha kuingiwa makubaliano kati ya Kampuni binafsi ya kuzalisha umeme ya Madope iliyopo wilayani Ludewa mkoani Njombe na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ya kukabidhi miundombinu ya kusafirisha na kusambaza umeme kwa Shirika hilo baada ya kusainiwa kwa mkataba kati ya pande hizo mbili.

Mhe. Kapinga amesema kuwa Serikali inathamini kazi kubwa inayofanywa na Kanisa Katoliki kwa kushirikiana na Serikali kwenye uwekezaji katika sekta mbalimbali.

Kwa upande wake Askofu wa jimbo la Njombe Eusebio Kyando ameupongezi Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa ushirikiano wao na kutoa fedha zilizowezesha kufanikisha mradi huo.

Kampuni ya Madope ni miongoni mwa wazalishaji wadogo wa umeme katika Wilaya ya Ludewa ambayo inamilikiwa kwa asilimia 55 na Kanisa Katoliki jimbo la Njombe.

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top