Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri wa Nishati Aweka Ukomo wa Kuagiza Vifaa Vya Ujenzi wa Miradi ya Nishati
Admin.Frank Mugogo 7099

Waziri wa Nishati Aweka Ukomo wa Kuagiza Vifaa Vya Ujenzi wa Miradi ya Nishati

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Merdad Kalemani ameagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme (TANESCO) kuweka mpango ambao utawezesha vifaa vyote vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme vinatengenezwa hapa nchini.

Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo katika Mkutano wake uliojumuisha viongozi wa Wizara, Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya REA uliofanyika tarehe 21 Oktoba 2019 katika Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo katika Mji wa Serikali wa Mtumba Jijini Dodoma. “Accessories kutoka nje ya nchi ni changamoto na zina mlolongo mrefu kutoka kuagizwa mpaka kufika nchini hivyo REA na TANESCO mjipange, kufikia tarehe 31 Desemba 2019 itakuwa mwisho wa kuagiza vifaa hivyo kutoka nje ya nchi” alisisitiza.

Waziri aliwaagiza REA na TANESCO kuyashawishi makampuni yanayozalisha vifaa yaliyopo nje ya nchi kufungua viwanda hivyo hapa nchini na kwamba tayari kuna kampuni zimeonesha nia ya kuanzisha viwanda hivyo nchini Tanzania. Aidha, Mh. Waziri aliitaka REB na Menejimenti ya REA kukutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kuweka mkakati wa pamoja ambao utasaidia kutolewa kwa wakati bandarini vifaa ambavyo vimeagizwa kutoka nje ya nchi ili kuweza kukamilisha miradi ya kusambaza umeme kwa wakati. “Wekeni mkakati wa pamoja na TRA kwa vifaa vyote vya miradi ya REA ambavyo vinaagizwa kutoka nje ya nchi visichelewe kutolewa bandarini”, alisisitiza.

Katika Mkutano huo, Mhe. Dkt. Merdad Kalemani amekubaliana na Bodi ya Nishati Vijijini kuwaweka katika uangalizi maalum wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza ambao utekelezaji wao umekuwa ukisuasua.

Dkt. Kalemani aliagiza ufanyike uchambuzi wa kina wa utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya III Mzunguko wa I ili kuwatambua wakandarasi wanaofanya vizuri na wale ambao utekelezaji wao umekuwa ni wa kusuasua ili waweze kusimamiwa kwa karibu kwa kuwekwa katika uangalizi maalum hatimaye waweze kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda unaotakiwa.

Mh. Waziri alisisitiza kuongeza usimamizi kwa wakandarasi ili kila mkandarasi aweze kuwasha umeme katika vijiji vitatu kila wiki na kuwa hilo litafanikiwa endapo wakandarasi wataongeza idadi ya wafanyakazi katika maeneo ya mradi. Aidha, aliagiza kuwa ikifika Desemba tarehe 31 Desemba 2019 kazi zote za marekebisho ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya II ambao ulikamilika Mwaka 2016 ziwe zimekamilika na makabidhiano yawe yamefanyika.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri aliagiza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya III Mzunguko wa II uanze Mwezi Januari Mwaka 2020 na kuharakisha maandalizi ya miradi ya ujazilizi katika vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme. Hata hivyo, alionya kuwa ufanyike uhakiki wa kina wa vijiji ambavyo vitapelekewa miradi ya umeme ili kujua mahitaji halisi.

Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Leonard Masanja alisema kuwa changamoto kubwa ya utekelezaji wa mradi unaoendelea hivi sasa inatokana na baadhi ya wakandarasi kuwa nyuma ya utekelezaji hivyo kusababisha vijiji vingi kutopelekewa umeme. “Tunaandaa Mzunguko wa II wa mradi tukiwa na madeni na muda uliobaki ni vigumu kwa wakandarasi kukamilisha kazi” alisisitiza.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top