Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri wa Nishati Aweka Ukomo wa Kuagiza Vifaa Vya Ujenzi wa Miradi ya Nishati
Admin.Frank Mugogo 6685

Waziri wa Nishati Aweka Ukomo wa Kuagiza Vifaa Vya Ujenzi wa Miradi ya Nishati

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Merdad Kalemani ameagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme (TANESCO) kuweka mpango ambao utawezesha vifaa vyote vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme vinatengenezwa hapa nchini.

Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo katika Mkutano wake uliojumuisha viongozi wa Wizara, Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya REA uliofanyika tarehe 21 Oktoba 2019 katika Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo katika Mji wa Serikali wa Mtumba Jijini Dodoma. “Accessories kutoka nje ya nchi ni changamoto na zina mlolongo mrefu kutoka kuagizwa mpaka kufika nchini hivyo REA na TANESCO mjipange, kufikia tarehe 31 Desemba 2019 itakuwa mwisho wa kuagiza vifaa hivyo kutoka nje ya nchi” alisisitiza.

Waziri aliwaagiza REA na TANESCO kuyashawishi makampuni yanayozalisha vifaa yaliyopo nje ya nchi kufungua viwanda hivyo hapa nchini na kwamba tayari kuna kampuni zimeonesha nia ya kuanzisha viwanda hivyo nchini Tanzania. Aidha, Mh. Waziri aliitaka REB na Menejimenti ya REA kukutana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kuweka mkakati wa pamoja ambao utasaidia kutolewa kwa wakati bandarini vifaa ambavyo vimeagizwa kutoka nje ya nchi ili kuweza kukamilisha miradi ya kusambaza umeme kwa wakati. “Wekeni mkakati wa pamoja na TRA kwa vifaa vyote vya miradi ya REA ambavyo vinaagizwa kutoka nje ya nchi visichelewe kutolewa bandarini”, alisisitiza.

Katika Mkutano huo, Mhe. Dkt. Merdad Kalemani amekubaliana na Bodi ya Nishati Vijijini kuwaweka katika uangalizi maalum wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza ambao utekelezaji wao umekuwa ukisuasua.

Dkt. Kalemani aliagiza ufanyike uchambuzi wa kina wa utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya III Mzunguko wa I ili kuwatambua wakandarasi wanaofanya vizuri na wale ambao utekelezaji wao umekuwa ni wa kusuasua ili waweze kusimamiwa kwa karibu kwa kuwekwa katika uangalizi maalum hatimaye waweze kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda unaotakiwa.

Mh. Waziri alisisitiza kuongeza usimamizi kwa wakandarasi ili kila mkandarasi aweze kuwasha umeme katika vijiji vitatu kila wiki na kuwa hilo litafanikiwa endapo wakandarasi wataongeza idadi ya wafanyakazi katika maeneo ya mradi. Aidha, aliagiza kuwa ikifika Desemba tarehe 31 Desemba 2019 kazi zote za marekebisho ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya II ambao ulikamilika Mwaka 2016 ziwe zimekamilika na makabidhiano yawe yamefanyika.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri aliagiza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya III Mzunguko wa II uanze Mwezi Januari Mwaka 2020 na kuharakisha maandalizi ya miradi ya ujazilizi katika vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme. Hata hivyo, alionya kuwa ufanyike uhakiki wa kina wa vijiji ambavyo vitapelekewa miradi ya umeme ili kujua mahitaji halisi.

Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Leonard Masanja alisema kuwa changamoto kubwa ya utekelezaji wa mradi unaoendelea hivi sasa inatokana na baadhi ya wakandarasi kuwa nyuma ya utekelezaji hivyo kusababisha vijiji vingi kutopelekewa umeme. “Tunaandaa Mzunguko wa II wa mradi tukiwa na madeni na muda uliobaki ni vigumu kwa wakandarasi kukamilisha kazi” alisisitiza.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top