Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini
Frank A. Mugogo 2676

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondosha madhara yatokanayo na njia zisizo salama. Madhara hayo ni pamoja na:

a)    Gharama kubwa za upatikanaji wa bidhaa hizo maeneo ya vijijini tofauti na bei elekezi;
b)    Gharama kubwa za usafiri hasa maeneo ya vijijini;
c)    Kuadimika kwa bidhaa hizo maeneo ya vijijini;
d)    Uuzaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta usio safi na salama (mapipa na madumu ya plastiki ndani ya nyumba);
e)    Milipuko ya moto ambayo inaweza kugharimu maisha ya wananchi na hivyo kupunguza nguvu kazi ya Taifa;
f)    Uharibifu wa mazingira unaotokana na bidhaa hizo kumwagika maeneo mbalimbali kwa sababu ya uhifadhi usiofaa;
g)    Kuikosesha Serikali mapato ambayo wauzaji wa mafuta (petroli na dizeli) hawalipi kodi na tozo mbalimbali; na
h)    Kuathiri afya kutokana na kuvuta hewa isiyo safi na salama kwa sababu ya kuhifadhi bidhaa hizo ndani ya nyumba.

Kwa kutambua hali hiyo, na kwa kuzingatia moja ya malengo ya Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015, ni wajibu wa Wakala kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa nishati na kwa bei nafuu katika maeneo yote ya nchi kwa njia iliyo salama.

Wakala wa Nishati Vijijini umetenga fedha kwa ajili ya kutoa mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Pamoja na tangazo hili, zimeambatanishwa nyaraka zifuatazo:
a)    Fomu ya Maombi ya Mkopo  wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini;
b)    Mwongozo wa Utoaji Mkopo wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vjijijini; na
c)    Tangazo la Fursa ya Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini.

Utaratibu utakaotumika kutekeleza mradi huu umeainishwa katika mwongozo wa    mradi    ambao    unapatikana    kupitia    tovuti    ya    Wakala    ambayo    ni www.rea.go.tz. 

Mwongozo huo umeainisha vigezo vitakavyotumika kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na hivyo kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa na Serikali. Mwongozo umeainisha namna ya kuomba mkopo, uidhinishwaji wa mkopo, vigezo vya mwombaji vya kiufundi na vya kifedha na masharti ya mkopo. Inasisitizwa waombaji kuzingatia matakwa ya mwongozo wakati wa kuwasilisha maombi ya mkopo.

Mwombaji atatakiwa kujaza fomu maalum ambayo inapatikana pia katika tovuti ya Wakala wa Nishati Vijijini (www.rea.go.tz). Maombi yaliyokamilika pamoja na viambatisho vyake yawasilishwe kwa njia ya zifuatazo:

Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Barabara ya Medeli,
S. L. P. 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Juu ya bahasha baada ya anuani ya Wakala iandikwe ‘Maombi ya Mkopo kwa Ajili ya Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini’.

Pia mwombaji anaweza kuwasilisha maombi kupitia njia ya mtandao kwa barua pepe: vituovyamafuta@rea.go.tz.

Mwisho wa kuwasilisha maombi ni kama ifuatavyo:
a)    Dirisha la maombi ya mkopo litafungwa pale ambapo idadi ya vituo 160 itakapofikiwa kulingana na bajeti iliyopo;
b)    Ikumbukwe kuwa kila baada ya miezi mitatu tathmini itafanyika kwa maombi yatakayokuwa yamepokelewa;
c)    Tathmini zitafanyika katika miezi ifuatavyo: 3,6,9 na wa 12; na
d)    Tunawahimiza waombaji kuwasilisha maombi yao mapema iwezekanavyo ili waweze kunufaika na fursa hii.

Kwa maelezo zaidi kutoka kwa Wakala wa Nishati Vijijini yawasilishwe kupitia barua pepe iliyotajwa hapo juu na kwa njia ya simu wasiliana na wafuatao:

Jina:    Mha. Kelvin Tarimo
Namba ya Simu:    0713 230358

Jina:    Mha. Ramadhani Mganga
Namba ya Simu:    0754 909237


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Medeli
S. L. P. 2153
DODOMA, TANZANIA

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top