Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini
Frank A. Mugogo 2445

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondosha madhara yatokanayo na njia zisizo salama. Madhara hayo ni pamoja na:

a)    Gharama kubwa za upatikanaji wa bidhaa hizo maeneo ya vijijini tofauti na bei elekezi;
b)    Gharama kubwa za usafiri hasa maeneo ya vijijini;
c)    Kuadimika kwa bidhaa hizo maeneo ya vijijini;
d)    Uuzaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta usio safi na salama (mapipa na madumu ya plastiki ndani ya nyumba);
e)    Milipuko ya moto ambayo inaweza kugharimu maisha ya wananchi na hivyo kupunguza nguvu kazi ya Taifa;
f)    Uharibifu wa mazingira unaotokana na bidhaa hizo kumwagika maeneo mbalimbali kwa sababu ya uhifadhi usiofaa;
g)    Kuikosesha Serikali mapato ambayo wauzaji wa mafuta (petroli na dizeli) hawalipi kodi na tozo mbalimbali; na
h)    Kuathiri afya kutokana na kuvuta hewa isiyo safi na salama kwa sababu ya kuhifadhi bidhaa hizo ndani ya nyumba.

Kwa kutambua hali hiyo, na kwa kuzingatia moja ya malengo ya Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015, ni wajibu wa Wakala kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa nishati na kwa bei nafuu katika maeneo yote ya nchi kwa njia iliyo salama.

Wakala wa Nishati Vijijini umetenga fedha kwa ajili ya kutoa mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Pamoja na tangazo hili, zimeambatanishwa nyaraka zifuatazo:
a)    Fomu ya Maombi ya Mkopo  wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini;
b)    Mwongozo wa Utoaji Mkopo wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vjijijini; na
c)    Tangazo la Fursa ya Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini.

Utaratibu utakaotumika kutekeleza mradi huu umeainishwa katika mwongozo wa    mradi    ambao    unapatikana    kupitia    tovuti    ya    Wakala    ambayo    ni www.rea.go.tz. 

Mwongozo huo umeainisha vigezo vitakavyotumika kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na hivyo kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa na Serikali. Mwongozo umeainisha namna ya kuomba mkopo, uidhinishwaji wa mkopo, vigezo vya mwombaji vya kiufundi na vya kifedha na masharti ya mkopo. Inasisitizwa waombaji kuzingatia matakwa ya mwongozo wakati wa kuwasilisha maombi ya mkopo.

Mwombaji atatakiwa kujaza fomu maalum ambayo inapatikana pia katika tovuti ya Wakala wa Nishati Vijijini (www.rea.go.tz). Maombi yaliyokamilika pamoja na viambatisho vyake yawasilishwe kwa njia ya zifuatazo:

Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Barabara ya Medeli,
S. L. P. 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Juu ya bahasha baada ya anuani ya Wakala iandikwe ‘Maombi ya Mkopo kwa Ajili ya Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini’.

Pia mwombaji anaweza kuwasilisha maombi kupitia njia ya mtandao kwa barua pepe: vituovyamafuta@rea.go.tz.

Mwisho wa kuwasilisha maombi ni kama ifuatavyo:
a)    Dirisha la maombi ya mkopo litafungwa pale ambapo idadi ya vituo 160 itakapofikiwa kulingana na bajeti iliyopo;
b)    Ikumbukwe kuwa kila baada ya miezi mitatu tathmini itafanyika kwa maombi yatakayokuwa yamepokelewa;
c)    Tathmini zitafanyika katika miezi ifuatavyo: 3,6,9 na wa 12; na
d)    Tunawahimiza waombaji kuwasilisha maombi yao mapema iwezekanavyo ili waweze kunufaika na fursa hii.

Kwa maelezo zaidi kutoka kwa Wakala wa Nishati Vijijini yawasilishwe kupitia barua pepe iliyotajwa hapo juu na kwa njia ya simu wasiliana na wafuatao:

Jina:    Mha. Kelvin Tarimo
Namba ya Simu:    0713 230358

Jina:    Mha. Ramadhani Mganga
Namba ya Simu:    0754 909237


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Medeli
S. L. P. 2153
DODOMA, TANZANIA

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top