Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini
Frank A. Mugogo 1867

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondosha madhara yatokanayo na njia zisizo salama. Madhara hayo ni pamoja na:

a)    Gharama kubwa za upatikanaji wa bidhaa hizo maeneo ya vijijini tofauti na bei elekezi;
b)    Gharama kubwa za usafiri hasa maeneo ya vijijini;
c)    Kuadimika kwa bidhaa hizo maeneo ya vijijini;
d)    Uuzaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta usio safi na salama (mapipa na madumu ya plastiki ndani ya nyumba);
e)    Milipuko ya moto ambayo inaweza kugharimu maisha ya wananchi na hivyo kupunguza nguvu kazi ya Taifa;
f)    Uharibifu wa mazingira unaotokana na bidhaa hizo kumwagika maeneo mbalimbali kwa sababu ya uhifadhi usiofaa;
g)    Kuikosesha Serikali mapato ambayo wauzaji wa mafuta (petroli na dizeli) hawalipi kodi na tozo mbalimbali; na
h)    Kuathiri afya kutokana na kuvuta hewa isiyo safi na salama kwa sababu ya kuhifadhi bidhaa hizo ndani ya nyumba.

Kwa kutambua hali hiyo, na kwa kuzingatia moja ya malengo ya Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015, ni wajibu wa Wakala kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa nishati na kwa bei nafuu katika maeneo yote ya nchi kwa njia iliyo salama.

Wakala wa Nishati Vijijini umetenga fedha kwa ajili ya kutoa mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Pamoja na tangazo hili, zimeambatanishwa nyaraka zifuatazo:
a)    Fomu ya Maombi ya Mkopo  wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini;
b)    Mwongozo wa Utoaji Mkopo wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vjijijini; na
c)    Tangazo la Fursa ya Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini.

Utaratibu utakaotumika kutekeleza mradi huu umeainishwa katika mwongozo wa    mradi    ambao    unapatikana    kupitia    tovuti    ya    Wakala    ambayo    ni www.rea.go.tz. 

Mwongozo huo umeainisha vigezo vitakavyotumika kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na hivyo kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa na Serikali. Mwongozo umeainisha namna ya kuomba mkopo, uidhinishwaji wa mkopo, vigezo vya mwombaji vya kiufundi na vya kifedha na masharti ya mkopo. Inasisitizwa waombaji kuzingatia matakwa ya mwongozo wakati wa kuwasilisha maombi ya mkopo.

Mwombaji atatakiwa kujaza fomu maalum ambayo inapatikana pia katika tovuti ya Wakala wa Nishati Vijijini (www.rea.go.tz). Maombi yaliyokamilika pamoja na viambatisho vyake yawasilishwe kwa njia ya zifuatazo:

Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Barabara ya Medeli,
S. L. P. 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Juu ya bahasha baada ya anuani ya Wakala iandikwe ‘Maombi ya Mkopo kwa Ajili ya Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini’.

Pia mwombaji anaweza kuwasilisha maombi kupitia njia ya mtandao kwa barua pepe: vituovyamafuta@rea.go.tz.

Mwisho wa kuwasilisha maombi ni kama ifuatavyo:
a)    Dirisha la maombi ya mkopo litafungwa pale ambapo idadi ya vituo 160 itakapofikiwa kulingana na bajeti iliyopo;
b)    Ikumbukwe kuwa kila baada ya miezi mitatu tathmini itafanyika kwa maombi yatakayokuwa yamepokelewa;
c)    Tathmini zitafanyika katika miezi ifuatavyo: 3,6,9 na wa 12; na
d)    Tunawahimiza waombaji kuwasilisha maombi yao mapema iwezekanavyo ili waweze kunufaika na fursa hii.

Kwa maelezo zaidi kutoka kwa Wakala wa Nishati Vijijini yawasilishwe kupitia barua pepe iliyotajwa hapo juu na kwa njia ya simu wasiliana na wafuatao:

Jina:    Mha. Kelvin Tarimo
Namba ya Simu:    0713 230358

Jina:    Mha. Ramadhani Mganga
Namba ya Simu:    0754 909237


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Medeli
S. L. P. 2153
DODOMA, TANZANIA

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top