Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini
Frank A. Mugogo 1251

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondosha madhara yatokanayo na njia zisizo salama. Madhara hayo ni pamoja na:

a)    Gharama kubwa za upatikanaji wa bidhaa hizo maeneo ya vijijini tofauti na bei elekezi;
b)    Gharama kubwa za usafiri hasa maeneo ya vijijini;
c)    Kuadimika kwa bidhaa hizo maeneo ya vijijini;
d)    Uuzaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta usio safi na salama (mapipa na madumu ya plastiki ndani ya nyumba);
e)    Milipuko ya moto ambayo inaweza kugharimu maisha ya wananchi na hivyo kupunguza nguvu kazi ya Taifa;
f)    Uharibifu wa mazingira unaotokana na bidhaa hizo kumwagika maeneo mbalimbali kwa sababu ya uhifadhi usiofaa;
g)    Kuikosesha Serikali mapato ambayo wauzaji wa mafuta (petroli na dizeli) hawalipi kodi na tozo mbalimbali; na
h)    Kuathiri afya kutokana na kuvuta hewa isiyo safi na salama kwa sababu ya kuhifadhi bidhaa hizo ndani ya nyumba.

Kwa kutambua hali hiyo, na kwa kuzingatia moja ya malengo ya Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015, ni wajibu wa Wakala kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa nishati na kwa bei nafuu katika maeneo yote ya nchi kwa njia iliyo salama.

Wakala wa Nishati Vijijini umetenga fedha kwa ajili ya kutoa mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Pamoja na tangazo hili, zimeambatanishwa nyaraka zifuatazo:
a)    Fomu ya Maombi ya Mkopo  wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini;
b)    Mwongozo wa Utoaji Mkopo wa Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vjijijini; na
c)    Tangazo la Fursa ya Ujenzi wa Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini.

Utaratibu utakaotumika kutekeleza mradi huu umeainishwa katika mwongozo wa    mradi    ambao    unapatikana    kupitia    tovuti    ya    Wakala    ambayo    ni www.rea.go.tz. 

Mwongozo huo umeainisha vigezo vitakavyotumika kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na hivyo kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa na Serikali. Mwongozo umeainisha namna ya kuomba mkopo, uidhinishwaji wa mkopo, vigezo vya mwombaji vya kiufundi na vya kifedha na masharti ya mkopo. Inasisitizwa waombaji kuzingatia matakwa ya mwongozo wakati wa kuwasilisha maombi ya mkopo.

Mwombaji atatakiwa kujaza fomu maalum ambayo inapatikana pia katika tovuti ya Wakala wa Nishati Vijijini (www.rea.go.tz). Maombi yaliyokamilika pamoja na viambatisho vyake yawasilishwe kwa njia ya zifuatazo:

Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Barabara ya Medeli,
S. L. P. 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Juu ya bahasha baada ya anuani ya Wakala iandikwe ‘Maombi ya Mkopo kwa Ajili ya Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini’.

Pia mwombaji anaweza kuwasilisha maombi kupitia njia ya mtandao kwa barua pepe: vituovyamafuta@rea.go.tz.

Mwisho wa kuwasilisha maombi ni kama ifuatavyo:
a)    Dirisha la maombi ya mkopo litafungwa pale ambapo idadi ya vituo 160 itakapofikiwa kulingana na bajeti iliyopo;
b)    Ikumbukwe kuwa kila baada ya miezi mitatu tathmini itafanyika kwa maombi yatakayokuwa yamepokelewa;
c)    Tathmini zitafanyika katika miezi ifuatavyo: 3,6,9 na wa 12; na
d)    Tunawahimiza waombaji kuwasilisha maombi yao mapema iwezekanavyo ili waweze kunufaika na fursa hii.

Kwa maelezo zaidi kutoka kwa Wakala wa Nishati Vijijini yawasilishwe kupitia barua pepe iliyotajwa hapo juu na kwa njia ya simu wasiliana na wafuatao:

Jina:    Mha. Kelvin Tarimo
Namba ya Simu:    0713 230358

Jina:    Mha. Ramadhani Mganga
Namba ya Simu:    0754 909237


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Barabara ya Medeli
S. L. P. 2153
DODOMA, TANZANIA

Rate article

3.1
Rate this article:
3.1

Share

Print
«July 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
24252627282930
1234
National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

The Government of the United Republic of Tanzania, in collaboration with various stakeholders has prepared the National Clean Cooking Strategy. The strategy aims to ensure that 80 percent of Tanzanians use clean cooking solutions by the year 2034.

Read more
567
891011121314
15161718192021
Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Ni vijiji 151 tu nchi nzima ndio ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 ambapo wilayani Ludewa mkoani Njombe vimebaki Vijiji nane.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top