Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
NORWAY YAISAIDIA TANZANIA SHILINGI BILIONI 200 KWA AJILI YA UMEME VIJIJINI
Host 12309

NORWAY YAISAIDIA TANZANIA SHILINGI BILIONI 200 KWA AJILI YA UMEME VIJIJINI

Serikali ya Tanzania imekamilisha makubaliano ya fedha za msaada wa Krona milioni 700, sawa na shilingi bilioni 200 za Tanzania, kutoka Serikali ya Norway, kwa ajili ya kupeleka umeme vijijini.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alisaini mkataba wenye makubaliano hayo, Aprili 9, 2013 Mjini Oslo Norway akiiwakilisha Serikali ya Tanzania, ambapo Serikali ya Norway iliwakilishwa na Waziri wake wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa, Bw. Heikki Holmas.

Zoezi la kusaini mkataba huo lilifanyika mwishoni mwa Mkutano ambao Waziri Muhongo alishiriki uliobeba dhima isemayo ‘Nishati na Maendeleo Kuanzia 2015’. Malengo mahsusi ya mkutano yalikuwa ni kufanya majumuisho ya majadiliano mbalimbali kuhusu nishati ambayo yamekuwa yakifanyika ulimwenguni kote na katika mitandao, na pia kutoa mapendekezo kuhusu nafasi ya nishati katika maendeleo kuanzia mwaka 2015.

Akizungumzia msaada huo, Prof. Muhongo alisema “sasa tunao uhakika wa kumaliza miradi ya umeme kwenye Wilaya mpya 13, zoezi litakalogharimu takribani shilingi bilioni 70 za kitanzania, na pia kukamilisha miradi mingine ya umeme vijijini”.

Kwa upande wake, Waziri Holmas alisema “kuwapatia watu waishio vijijini huduma ya umeme ni sawa na kuwapatia Watanzania wengi uwezekano wa kuondokana na matumizi ya nishati zenye uharibifu kama mafuta ya taa na dizeli.” Alifafanua kuwa msaada huo unalenga kuleta usawa kwa vitendo, ambao utainua hali ya maisha haraka na kuleta njia mbadala za kujipatia kipato kwa wananchi wa vijijini.

Alisema, zaidi ya asilimia 90 ya msaada uliotolewa itatumika kuweka umeme kwa kuongeza miundombinu ya usambazaji wa umeme, ambapo kwa mujibu wake ndiyo namna nzuri zaidi ya kuyafikia maeneo ya vijijini kwa huduma husika, kulingana na uzoefu.

Profesa Muhongo alisema Tanzania imedhamiria kuongeza huduma ya upatikanaji wa nishati ya umeme kwa Watanzania kutoka asilimia 18.4 hadi 30 kwa ngazi ya taifa, na kutoka asilimia 6.5 hadi 15 kwa maeneo ya vijijini.

Baada ya Mkutano na makubaliano hayo, Waziri Muhongo ameendelea na safari yake katika Mji wa Brussels, Ujerumani akiendelea na zoezi la kutafuta fedha za miradi mbalimbali ya umeme.

Imeandaliwa na:

Fadhili P. Kilewo
Mkuu wa Idara ya Habari
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
17
REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

Read more
1819
Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruzuku ya shilingi 7,500 yanayosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kulinda afya, kuokoa misitu na kuhifadhi mazingira.

Read more
2021
REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top