Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Uzinduzi wa Tovuti ya Miradi Midogo ya Umeme (Minigrids Portal)
Aodax K. Nshala 5571

Uzinduzi wa Tovuti ya Miradi Midogo ya Umeme (Minigrids Portal)

Event date: 8/11/2016 Export event

Kwa Ushirikiano na Benki ya Dunia Kupitia International Finance Corporation (IFC)

Serikali ya Jamhuri ya Muugano wa Tanzania imezindua tovuti inayotoa taarifa za fursa na taratibu za uwekezaji kwenye miradi midogo ya umeme nje ya gridi ya Taifa.

Uzinduzi wa tovuti hiyo ulifanyika tarehe 11 Agosti, 2016 katika Ofisi za Benki ya Dunia Tanzania. Lengo la tovuti hiyo ni kutoa taarifa ambazo zitawawezesha waendelezaji wa miradi ya nishati bora vijijini, wawekezaji mbalimbali pamoja na wadau wengine kupata taarifa sahihi ambazo zitachangia katika kuongeza wigo wa usambazaji na upatikanaji wa nishati bora vijijini.

Tovuti hiyo inatoa taarifa za kina kwa waendelezaji na wawekezaji kwenye miradi midogo ya nishati jadidifu nchini Tanzania.

Uanzishwaji wa tovuti hii umefanyika chini ya mradi wa SREP (Scaling-Up Renewable Energy Program) ambao unachochea uwekezaji kwenye nishati jadidifu ikijumuisha miradi midogo ya umeme (minigrids).

Tovuti hiyo, www.minigrids.go.tz inasimamiwa na kuhifadhiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na taarifa zake zinaratibiwa kwa ushirikiano wa uwakilishi wa wadau wengine ambao ni Wizara ya Nishati na Madini (MEM), EWURA, NEMC, TAREA, TBS pamoja na TANESCO.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top