Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UZINDUZI WA UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KIGOMA
Aodax K. Nshala 18414

UZINDUZI WA UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KIGOMA

UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KATIKA MKOA WA KIGOMA NA UKAGUZI WA MIRADI YA UMEME VIJIJINI KATIKA MIKOA YA KATAVI NA RUKWA

Waziri wa Nishati, Mh. Dk, Medard M. Kalemani (Mb) amezindua utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Kigoma na kukag2ua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini katika Mikoa ya Katavi na Rukwa. Mh. Waziri alifanya uzinduzi huo tarehe 29 Januari, 2018 katika kijiji cha Mabamba, Kata ya Mabamba, Wilaya ya Kibondo.

Mradi huu unajumuisha vipengele-mradi vitatu vya Grid Extension, Densification ambayo inalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme kwenye vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme lakini baadhi ya vijiji na vitongoji havikuunganishiwa umeme. Kipengele-mradi cha tatu kinahusisha usambazaji wa nishati jadidifu kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi.

Utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Kigoma utahusisha vipengele vyote vitatu vya mradi. Mradi huu utatekelezwa kwa vipindi viwili tofauti. Sehemu ya awali itahusisha upelekaji umeme katika vijiji 149 vya Mkoa wa Kigoma kwa gharama ya Shilingi Bilioni 60.5. Utekelezaji wa sehemu hii ya kwanza umeanza Mwezi Februari, 2018 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Machi 2019. Katika Mkoa wa Kigoma, utekelezaji wa miradi umegawanywa katika Loti mbili. Loti Na. 1 inahusu Wilaya za Kibondo na Kakonko. Loti Na.2 inahusu Wilaya za Kasulu, Buhigwe, Kigoma Vijijini na Uvinza. Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Loti Na. 1 ni M/s Urban & Rural Engineering Services Ltd. Wizara ipo katika hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi wa Loti Na.2. Mchakato wa manunuzi utakapokamilika, Mkandarasi huyo ataanza kazi mara moja.

Aidha, sehemu ya pili ya mradi huu wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu itaanza kutekelezwa baada ya sehemu ya kwanza kukamilika ifikapo Mwezi Machi 2019 ambapo vijiji 91 vya Mkoa wa Kigoma vitapatiwa umeme na hivyo kufikisha umeme katika vijiji vyote ifikapo Mwaka 2021.

Tahere 30 Januari, 2018, Mh. Waziri wa Nishati alikagua miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Katavi. Alianza kwa kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha kufua umeme kilichopo Mjini Mpanda . Akiwa Mjini Inyonga, katika Wilaya ya Mlele, Mh. Waziri alikagua ujenzi wa kituo cha kufua umeme kwa ajili ya matumizi katika wilaya hiyo. Pia Mh. Waziri aliwahutubia wananchi wa Wilaya ya Mlele na kuwaeleza taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na mfumo wa kulipia miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Tahere 31 Januari, 2018, Mh. Waziri wa Nishati alikagua miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Rukwa. Kwa nyakati tofauti, Mh. Waziri aliwahutubia wananchi wa Kijiji cha Ntendo, Wilaya ya Sumbawanga Mjini na kuwaeleza taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na taratibu za kulipia ili kuunganishwa na huduma ya umeme kwenye miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na hata baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mh. Waziri alihitimisha kwa kuwahutubia wananchi wa Kijiji cha Miangalua, Wilaya ya Sumbawanga Vijijini. Kama alivyohutubia sehemu za awali, Mh. Waziri aliwaeleza wananchi taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na taratibu za kulipia ili kuunganishwa na huduma ya umeme kwenye miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na hata baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«May 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
27282930123
45678
Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Wakandarasi Wanaotekeleza Miradi Ya REA Watakiwa Kumaliza Miradi Kwa Wakati

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, leo tarehe 8 Mei, 2026 imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini katika Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kupata taarifa ya utekelezani wa miradi hiyo.

Read more
910
11121314151617
181920212223
REA na Shirika la Mzinga Kushirikiana Kuendeleza Teknolojia Za Nishati Safi ya Kupikia

REA na Shirika la Mzinga Kushirikiana Kuendeleza Teknolojia Za Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Mzinga leo wamesaini hati ya makubaliano ya ushirikiano yanayolenga kuimarisha ushirikiano katika Utafiti, Teknolojia, Uzalishaji na Usambazaji wa nishati safi ya kupikia.

Read more
24
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top