Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UZINDUZI WA UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KIGOMA
Aodax K. Nshala 17874

UZINDUZI WA UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KIGOMA

UZINDUZI WA MRADI KABAMBE WA UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU KATIKA MKOA WA KIGOMA NA UKAGUZI WA MIRADI YA UMEME VIJIJINI KATIKA MIKOA YA KATAVI NA RUKWA

Waziri wa Nishati, Mh. Dk, Medard M. Kalemani (Mb) amezindua utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Kigoma na kukag2ua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini katika Mikoa ya Katavi na Rukwa. Mh. Waziri alifanya uzinduzi huo tarehe 29 Januari, 2018 katika kijiji cha Mabamba, Kata ya Mabamba, Wilaya ya Kibondo.

Mradi huu unajumuisha vipengele-mradi vitatu vya Grid Extension, Densification ambayo inalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme kwenye vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme lakini baadhi ya vijiji na vitongoji havikuunganishiwa umeme. Kipengele-mradi cha tatu kinahusisha usambazaji wa nishati jadidifu kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi.

Utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Kigoma utahusisha vipengele vyote vitatu vya mradi. Mradi huu utatekelezwa kwa vipindi viwili tofauti. Sehemu ya awali itahusisha upelekaji umeme katika vijiji 149 vya Mkoa wa Kigoma kwa gharama ya Shilingi Bilioni 60.5. Utekelezaji wa sehemu hii ya kwanza umeanza Mwezi Februari, 2018 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Machi 2019. Katika Mkoa wa Kigoma, utekelezaji wa miradi umegawanywa katika Loti mbili. Loti Na. 1 inahusu Wilaya za Kibondo na Kakonko. Loti Na.2 inahusu Wilaya za Kasulu, Buhigwe, Kigoma Vijijini na Uvinza. Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Loti Na. 1 ni M/s Urban & Rural Engineering Services Ltd. Wizara ipo katika hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi wa Loti Na.2. Mchakato wa manunuzi utakapokamilika, Mkandarasi huyo ataanza kazi mara moja.

Aidha, sehemu ya pili ya mradi huu wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu itaanza kutekelezwa baada ya sehemu ya kwanza kukamilika ifikapo Mwezi Machi 2019 ambapo vijiji 91 vya Mkoa wa Kigoma vitapatiwa umeme na hivyo kufikisha umeme katika vijiji vyote ifikapo Mwaka 2021.

Tahere 30 Januari, 2018, Mh. Waziri wa Nishati alikagua miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Katavi. Alianza kwa kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha kufua umeme kilichopo Mjini Mpanda . Akiwa Mjini Inyonga, katika Wilaya ya Mlele, Mh. Waziri alikagua ujenzi wa kituo cha kufua umeme kwa ajili ya matumizi katika wilaya hiyo. Pia Mh. Waziri aliwahutubia wananchi wa Wilaya ya Mlele na kuwaeleza taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na mfumo wa kulipia miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Tahere 31 Januari, 2018, Mh. Waziri wa Nishati alikagua miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Rukwa. Kwa nyakati tofauti, Mh. Waziri aliwahutubia wananchi wa Kijiji cha Ntendo, Wilaya ya Sumbawanga Mjini na kuwaeleza taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na taratibu za kulipia ili kuunganishwa na huduma ya umeme kwenye miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na hata baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mh. Waziri alihitimisha kwa kuwahutubia wananchi wa Kijiji cha Miangalua, Wilaya ya Sumbawanga Vijijini. Kama alivyohutubia sehemu za awali, Mh. Waziri aliwaeleza wananchi taratibu za utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Umeme Vijijini ikiwa ni pamoja na taratibu za kuunganisha kwenye nyumba. Pia Mh.Waziri alifafanua gharama na taratibu za kulipia ili kuunganishwa na huduma ya umeme kwenye miradi ya umeme vijijini wakati wa utekelezaji wa mradi na hata baada ya kukamilika utekelezaji wa miradi hiyo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top