Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme
Admin.Frank Mugogo 7361

Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo amevipongeza viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa uzalishaji wa vifaa kwa kiwango kikubwa unaochochea ukuaji wa sekta ya nishati nchini.

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ilifanya ziara ya kutembelea viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Njombe na Iringa ili kujionea shughuli za uzalishaji vifaa hivyo.
Katika ziara hiyo, wamiliki wa viwanda vya vifaa vya umeme wameahidi kuendelea kuzalisha vifaa hivyo kwa kiwango kikubwa ili kukidhi mahitaji ya miradi ya umeme nchini.

Wakili Kalolo alisema ameridhishwa na kasi ya uzalishaji wa vifaa katika viwanda hivyo na kusisitiza umuhimu wake katika kufanikisha kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijijni ambayo inaendelea nchini, ambapo mpaka sasa ni vijiji 7400 kati ya 12,268 vimeunganishwa na huduma ya umeme.
“Ziara hii imetusaidia kujua changamoto wanazokumbana nazo wazalishaji wa vifaa vya umeme, lakini pia naweza kuthibitisha uwezo wao baada ya kutembelea viwanda hivi, ni wazi kwamba suala la nguzo za umeme tunajitosheleza kwa viwanda vyetu, suala la mita na waya sio changamoto, vyote vinazalishwa ndani ya nchi”, aliongeza Wakili Kalolo.

Pia Wakili Kalolo amewapongeza wamiliki wa viwanda hivyo kwa kuajiri wafanyakazi wazawa kwa wingi na kuwataka kuendelea kuongeza wafanyakazi wanaopatikana hapa hapa nchini Tanzania. Wakili Kalolo aliongeza kusema kuwa, Serikali imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuhakikisha kuwa juhudi za Rais John Magufuli kwamba Serikali itafikia uchumi wa kati kufikia Mwaka 2025.

Akielezea umuhimu wa viwanda hivyo katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga amesema watengenezaji wa vifaa vinavyotumika katika miradi ya umeme, kama vile mita, waya, transfoma, nguzo na vingine vingi ni wadau muhimu sana katika kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo vijijini kupitia nishati ya umeme.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top