Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Waziri wa Nishati Zanzibar Aipa Kongole REA
Frank A. Mugogo 96

Waziri wa Nishati Zanzibar Aipa Kongole REA

Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe. Shaib Kaduara ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhakikisha huduma za Nishati zinafika katika maeneo yote ya Vijiji Tanzania Bara.

Ametoa pongezi hizo Jijini Dar es Salaam Oktoba 25, 2024 alipotembelea Banda la Wakala kabla ya kufunga Kongamano la 10 la Jotoardhi (ARGeo-C10).

Mhe. Kaduara aliisisitiza REA kuhakikisha inaongeza nguvu katika suala la uhamasishaji ili kuwezesha wananchi umuhimu wa kubadilika na kuachana na matumizi ya nishati ambazo sio safi na salama kwa afya zao na kwa mazingira.

"Hongereni mnafanya kazi nzuri, muhimu ni kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi waelewe umuhimu wa kubadilika na kuachana na matumizi ya Nishati chafu," alielekeza.

Awali akitoa maelezo ya majukumu ya REA, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage alisema Wakala unatekeleza Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) ambao ulizinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhandisi Mwijage amesema REA inatekeleza program mbalimbali ili kuhakikisha wananchi hususan wa maeneo ya vijijini wanapunguza na baadae kuachana kabisa na matumizi ya nishati chafu za kupikia ikiwemo kuni na mkaa.

"Tumeingia makubaliano na wasambazaji wa mitungi ya gesi ya kupikia ambapo kwa mwaka huu 2024/2025 tunatoa mitungi zaidi ya laki nne kwa bei ya ruzuku ya asilimia 50," amesema.

Ameongeza kuwa majadiliano yanaendelea na watengenezaji wa majiko banifu ambapo kwa awamu ya kwanza majiko yapatayo 200,000 yatatolewa kwa bei ya ruzuku ya hadi asilimia 75.

Aidha alizungumzia suala la usambazaji wa umeme maeneo ya vijijini ambapo alisema hadi kufikia Desemba mwaka huu vijiji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimeunganishwa na umeme.

"Kwa sasa zaidi ya asilimia 98 ya vijiji vyote Tanzania Bara vimeunganishwa na umeme na sasa tumeanza kusambaza umeme vitongojini," amesema Mhandisi Mwijage.

Mhandisi Mwijage amesema Wakala unashiriki Kongamano la 10 la Jotoardhi kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya Nishati Jadidifu hasa ikizingatiwa kuwa Jotoardhi ni aina moja ya nishati jadidifu.

Amesema REA inafadhili miradi mbalimbali ya Nishati Jadidifu na kwamba kwa miradi ya upepo, jua na maporomoko ya maji Watanzania wengi wamejitokeza kushirikiana na Serikali kuitekeleza.

Hata hivyo amesema kwa Nishati ya Jotoardhi bado wananchi hawajawa na mwamko wa kutosha na kwamba kupitia kongamano na uhamasishaji unaofanywa na Serikali wanananchi watahamasika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top