Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi
Mohamed Saif 29

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Wabunge waimwagia sifa REA

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema hayo Aprili 22, 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati anawasilisha taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 katika Bunge la 13 Mkutano wa Tatu, Kikao cha Kumi na Nne.

“Mwelekeo wa Serikali ni kuhakikisha umeme unafikishwa katika vitongoji vyote Tanzania Bara na ili kufikia azma hiyo, Serikali ilianza utekelezaji wa mradi mkubwa wa kupeleka umeme katika Vitongoji 9,009 ambao utakamilika katika kipindi cha miaka mitatu ijayo,” amesema Waziri Ndejembi.

Amefafanua kuwa miradi inayoendelea kutekelezwa ya kupeleka umeme vitongojini itawezesha vitongoji 50,453 sawa na asilimia 78.4 ya vitongoji vyote vya Tanzania Bara kufikishiwa huduma ya umeme ifikapo mwaka 2028, hatua ambayo itachochea kasi ya ukuaji wa uchumi vitongojini.

Waziri Ndejembi ametaja hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali katika kupeleka nishati vijijini ni kuwa ni pamoja na kuanza utekelezaji wa mradi wa kuongeza uunganishaji wa wateja katika vitongoji (Universal Hamlet Eletrification and Last Mile Customers Connectivity) katika mikoa ya Pwani, Morogoro na Dodoma ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mahsusi wa Nishati wa Taifa (National Energy Compact) ulioridhiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika (Mission 300) mwezi Januari, 2025.

Hatua nyingine ni utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji 3,060 sawa na vitongoji 15 kwa kila Jimbo ambao amesema umefikia 80% ya utekelezaji.

“Serikali iliendelea na utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme katika Vitongoji vya Mikoa ya Songwe, Kigoma na Lindi pamoja na maeneo ya migodi midogo ikiwemo iliyopo Chunya (Mbeya) na Kwa Msisi Handeni (Tanga) na viwanda na kilimo katika Mikoa ya Ruvuma, Njombe, Mbeya na Rukwa ili kuchochea shughuli za kiuchumi katika mikoa hiyo, ambapo utekelezaji upo hatua mbalimbali,” amebainisha Waziri Ndejembi.

Katika kuhakikisha kuwa maeneo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa yanafikiwa na huduma za umeme Waziri Ndejembi amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) iliendelea na utekelezaji wa mradi wa kusambaza mifumo ya jua inayojitegemea (Solar Home System-SHS) katika makazi 20,000 katika visiwa vidogo 143 vilivyopo katika Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika ambapo hadi Machi, 2026 jumla ya makazi 1,302 yalikuwa yamefungiwa mifumo hiyo. 

Aidha, akizungumzia eneo la Nishati Safi ya Kupikia, Waziri Ndejembi amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, inaendelea na utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024 - 2034) uliozinduliwa mwezi Mei, 2024, wenye lengo la kuhakikisha angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

“Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kiafya na kimazingira na kuwezesha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi na katika taasisi hususan, zinazohudumia watu zaidi ya 100,” amefafanua Waziri Ndejembi.

Amesema kuwa kutokana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali, matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini yameendelea kuimarika kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 28.6 ya watanzania wenye nishati safi ya kupikia mwaka 2025, hatua ambayo amesema inachangia katika kupunguza uharibifu wa mazingira dhidi ya matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia na pia kulinda afya za wananchi dhidi ya matumizi ya nishati zisizo safi za kupikia.

“Kwa namna ya kipekee, nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongea Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa maono na uongozi wake uliotuwezesha kuwa na mwelekeo huu wa kitaifa wa kuhakikisha wananchi wetu wanatumia nishati safi ya kupikia, ajenda ambayo imempa heshima ya kuwa kinara wa nishati safi ya kupikia Barani Afrika na kimataifa,” amesema Waziri Ndejembi.

Kwa nyakati tofauti wakichangia katika hotuba hiyo ya Nishati, wabunge waliipongeza REA kwa hatua iliyofikia ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme na miradi ya nishati safi ya kupikia sambamba na

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top