Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini
Aodax K. Nshala 524

Serikali Kuongeza Matumizi ya Gesi ya Kupikia Nchini

Mitungi 83,500 Yenye Thamani ya Bilioni 3.5 Imetolewa na REA Mpaka Sasa

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali inayo mikakati ya kuhakikisha inaongeza matumizi ya gesi ya kupikia nchini.
 
Ameyasema hayo leo wakati wa mkutano na wananchi wa Mbinga kuhusu nishati safi ya kupikia ambao uliambatana na ugawaji ma mitungi ya gesi Zaidi ya 1500 kwa wananchi wa eneo hilo.
 
“Mpaka sasa kupitia REA tumeshatoa mitungi ya ruzuku 83,500 yenye thamani ya bilioni 3.5 na mwaka huu wa fedha tutatoa mitungi mingine 452,445 yenye thamani ya bilioni 10 ikiwa nia yetu na dhamira yetu ni kupunguza matumizi ya gharama ya kwanza".
 
Aawali akitoa mada kuhusu hatua zilizokwishachukuliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutekeleza maono hayo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anayetaka kufikia 2030 zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, Kaimu Meneja Msaidizi wa Kiufundi REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya amesema Wakala umesambaza zaidi ya majiko banifu 200,000 kwa wananchi.
 
Ameongeza pia Serikali kupitia REA imetenga Shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kuwezesha taasisi zinazohudumia watu Zaidi ya 300 kutumia nishati safi ya kupikia.
 

Imetolewa na:
Iddy M. Mwema
imwema@rea.go.tz
Afisa Habari
REA

Share

Print
«April 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
303112
REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

REA Yatangaza Mafanikio Makubwa Ya Usambazaji Wa Nishati Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetangaza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini, huku ukieleza kuwa vijiji vyote nchini tayari vimefikishiwa umeme na sasa nguvu kubwa imeelekezwa katika vitongoji.

Read more
345
67891011
REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

REA Yawasha Umeme Vitongoji 307 Namtumbo

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Read more
12
1314151617
REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

REA Yachochea Uwekezaji Mkoa Wa Mwanza – RC Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vijiji pamoja na pembezoni mwa mji hali iliyochochea kuongezeka kwa uwekezaji maeneo ya vijijini.

Read more
1819
2021
Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Dkt. Mataragio Atembelea Banda la REA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio  akitazama hali ya usambazaji umeme vitongojini kupitia Mfumo maalum wa Mawasiliano uliyobuniwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwaajili ya kuonyesha hali ya usambazaji umeme na mipango iliyopo maarufu kama REA Digital Platform alipotembelea Banda la REA

Read more
22
Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Vitongoji Vyote Tanzania Bara Kuwa Na Umeme Ifikapo Mwaka 2030- Waziri Ndejembi

Serikali imedhamiria kuhakikisha vitongoji vyote 64,359 vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme ifikapo mwaka 2030 ili kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii vitongojini pamoja na utoaji wa huduma bora katika maeneo hayo.

Read more
23242526
27282930123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top