Serikali imetoa takribani Shilingi Bilioni 50 kwa ajili ya kuwawezesha waendelezaji wadodo wadogo kwenye miradi ya nishati jadidifu, ambazo ni umeme unaozalishwa kutokana na vyanzo vya jua, upepo, maporomoko ya maji pamoja na tungamo taka katika maeneo yaliyopo vijijini Tanzania Bara.
Serikali imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye vijiji na mitaa viliyopo pembezoni mwa miji na majiji.Uzinduzi huo umefanyika na Waziri wa Nishati Mh. Dk Medard Kalemani pamoja na Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu katika maeneo ya Kigamboni, Kisarawe, Mkuranga, Kibaha, Mlandizi, Bagamoyo na Chalinze.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo amevipongeza viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa uzalishaji wa vifaa kwa kiwango kikubwa unaochochea ukuaji wa sekta ya nishati nchini.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amesema miradi ya kusambaza umeme vijijini inayotekelezwa katika wilaya na mikoa yote Tanzania Bara itafanikisha azma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo Mwaka 2025.
Waziri wa Nishati Mh. Dk. Merdad Kalemani amewataka wadau wote wanaoshiriki katika utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza kushiriki kikamilifu na kuharakisha utekelezaji wake.
Uploaded is the REPDF Lot 1 Consultant Database.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dr. John Pombe Magufuli amemteua Wakili Julius B. Kalolo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini.
Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini imekutana wa Wakandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I katika Ukumbi wa Hazina, Dodoma kujadili changamoto mbalimbali zinazoweza kuchelewesha utekelezaji wa Mradi.